Yaliyomo
JUMA LA DESEMBA 25-31, 2017
3 Imba kwa Shangwe na Sauti Kubwa!
Sikuzote kuimba kumekuwa sehemu muhimu ya ibada ya watu wa Yehova. Hata hivyo, huenda wengine wakaaibika kuimba hadharani. Tunaweza kufanya nini ili kushinda woga wa kutumia sauti zetu kumwimbia Yehova sifa? Makala hii inatupatia sababu nzuri za kuimba kwa shangwe na sauti kubwa na inatoa mapendekezo ya jinsi ya kuboresha sauti zetu.
JUMA LA JANUARI 1-7, 2018
8 Je, Unamfanya Yehova Kuwa Kimbilio Lako?
JUMA LA JANUARI 8-14, 2018
13 Iga Haki na Rehema ya Yehova
Tunaweza kujifunza mambo muhimu kutokana na mpango wa majiji ya makimbilio katika Israeli la kale. Katika makala ya kwanza, chunguza uone jinsi ambavyo mtenda-dhambi anaweza kumfanya Yehova kuwa kimbilio lake leo. Katika makala ya pili, ona jinsi mfano wa Yehova unavyotusaidia tuwasamehe wengine, tuheshimu uhai, na kutenda kwa haki.
18 ‘Mwenye Ukarimu Atabarikiwa’
JUMA LA JANUARI 15-21, 2018
JUMA LA JANUARI 22-28, 2018
25 Usiruhusu Chochote Kikunyang’anye Tuzo
Makala hizi mbili zinategemea shauri lililoongozwa na roho ambalo Paulo aliwaandikia Wakristo Wakolosai. Makala ya kwanza inaeleza mambo tunayopaswa kufanya tunaposikia maoni ya ulimwengu yanayoonekana kuwa yenye kuvutia au kusadikisha. Makala ya pili inatukumbusha jinsi ya kuepuka mitazamo inayoweza kufanya tukose baraka ambazo Yehova ameahidi.