Yaliyomo
JUMA LA OKTOBA 29, 2018–NOVEMBA 4, 2018
3 “Ikiwa Mnajua Mambo Haya, Mtakuwa Wenye Furaha Mkiyatenda”
Ujuzi hauwezi kutunufaisha ikiwa hatuutumii. Lakini tunahitaji sifa ya unyenyekevu ili tutumie yale tunayojifunza. Makala hii itatutia moyo tuendelee kuwa wanyenyekevu kwa kuiga mifano inayopatikana katika Biblia ya wale ambao waliwahubiria watu wa namna zote, walisali kwa ajili ya wengine, na kumngojea Yehova atende.
8 Enyi Wakristo Wenye Umri Mkubwa—Yehova Anathamini Sana Ushikamanifu Wenu
JUMA LA NOVEMBA 5-11, 2018
12 Endeleeni Kuonyeshana Upendo—Unajenga
Katika nyakati hizi zilizo ngumu, ni rahisi sana kuvunjika moyo au kulemewa na changamoto za maisha. Yehova na Yesu wanatusaidia kukabiliana na hali hizo. Lakini sisi sote tuna jukumu la kuwafariji na kuwatia moyo wengine. Makala hii inatuonyesha jinsi tunavyoweza kujengana katika upendo.
JUMA LA NOVEMBA 12-18, 2018
17 Wenye Furaha Ni Watu Wanaomtumikia “Mungu Mwenye Furaha”
Yehova ni Mungu mwenye furaha anayetaka watumishi wake wawe na furaha. Lakini tunawezaje kuwa na furaha licha ya matatizo au changamoto tunazokabili katika ulimwengu wa Shetani? Katika Mahubiri ya Mlimani, Yesu alitupatia ushauri mzuri sana unaoweza kutusaidia kuwa na furaha ya kudumu.
JUMA LA NOVEMBA 19-25, 2018
23 Mweza Yote, Lakini Mwenye Ufikirio
JUMA LA NOVEMBA 26, 2018–DESEMBA 2, 2018
28 Mwige Yehova kwa Kuwaonyesha Wengine Ufikirio na Fadhili
Katika ulimwengu ambao watu wanazidi kuonyesha roho ya ubinafsi, upendo uliopo katika kutaniko la Kikristo unaonekana waziwazi. Kuwaonyesha wengine ufikirio ni sehemu ya upendo huo. Nasi tutazungumzia sifa hiyo katika makala hizi mbili. Kwanza, tutachunguza mfano mzuri sana ambao Yehova ametuwekea wa kuwaonyesha wengine ufikirio. Kisha tutazungumzia baadhi ya mambo tunayoweza kufanya ili tumwige.