Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/14 uku. 2
  • Sanduku la Swali

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sanduku la Swali
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2014
  • Habari Zinazolingana
  • “Basi, Nendeni Mkafanye Wanafunzi”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
  • Jinsi ya Kumsaidia Mwanafunzi wa Biblia Afikie Hatua ya Ubatizo—Sehemu ya Kwanza
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
  • Jinsi ya Kumsaidia Mwanafunzi wa Biblia Afikie Hatua ya Ubatizo—Sehemu ya Pili
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2020
  • Wasaidie Wanafunzi Wako wa Biblia Wafikie Ubatizo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2014
km 4/14 uku. 2

Sanduku la Swali

● Tunawezaje kuwasaidia wanafunzi wetu wa Biblia wastahili kubatizwa na kuwa wanafunzi wa Yesu Kristo?

Tunaweza kufanikiwa kuwasaidia kwa (1) kuongoza funzo la Biblia la kawaida na lenye maendeleo, (2) kuwatia moyo wahudhurie mikutano yote mitano ya kutaniko na watoe maelezo kwa ukawaida, na (3) mara tu wanapostahili kulingana na Maandiko, kuwasaidia na kuwazoeza washiriki kwa bidii katika utumishi wa shambani.

Yesu Kristo aliwatuma wanafunzi wake wakafanye wanafunzi, wawabatize, na kuwafundisha kushika mambo yote ambayo aliwaamuru. Bado kazi hiyo ni muhimu hadi leo, kama maneno ya Yesu yanavyoonyesha: “Na, tazama! mimi nipo pamoja nanyi siku zote mpaka umalizio wa mfumo wa mambo.”—Mt. 28:19, 20.

Mwanafunzi ni mtu anayekubali na kuendeleza mafundisho ya mwingine. Kwa hiyo, wale wanaobatizwa wanapaswa kuwa wamepata ujuzi wa msingi wa kweli ya Biblia, na tayari wanaonyesha katika maisha yao kwamba wanaelewa na wanafuata viwango vya Yehova vya uadilifu. Kwa kuongezea, wanafunzi wa Yesu Kristo wanatambua tengenezo la Yehova linaloonekana, na mamlaka ya Yesu Kristo kupitia “mtumwa mwaminifu na mwenye busara.” (Mt. 24:45-47; Mdo. 1:8) Kwa kuwa wanajua mwisho u karibu, wanajiunga na watumishi wa Yehova katika kufanya kazi ambayo Yesu alianzisha na kuwaagiza wafuasi wake waendelee kuifanya. (Luka 8:1; Mt. 24:14) Ubatizo wa wanafunzi hao ni ishara ya nje ya kwamba wamejiweka wakfu kwa Yehova, kwa nafsi yote.—Linganisha na Zaburi 40:8.

Ni vizuri kukumbuka kwamba, tunawasaidia wanafunzi wa Biblia kuwa wanafunzi wa Yesu Kristo na si wanafunzi wetu. Kwa hiyo basi, ikiwa hali zetu za kibinafsi, muda tunaopatikana, uwezo wetu wa kufundisha, au kwa sababu nyingine muhimu tunaona hatutaweza kumsaidia mwanafunzi wa Biblia kufanya maendeleo yanayohitajika, tunapaswa kuongea na wazee kuhusu jambo hilo. Wao wanaweza kutupa ushauri unaofaa ambao utachangia katika maendeleo ya kiroho ya mwanafunzi huyo, kama inavyoelezwa na maneno ya Paulo katika 1 Wakorintho 3:5-9.

Funzo la Biblia la nyumbani liendelezwe mpaka mwanafunzi amalize kusoma vitabu vyote viwili, yaani Biblia Inafundisha Nini Hasa? na “Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu,” hata kama mwanafunzi huyo amestahili na amebatizwa kabla ya kumaliza kujifunza vitabu hivyo. Ikiwa vitabu hivyo vyote viwili au kimojawapo havipatikani katika lugha ya mwanafunzi, mnaweza kutumia kitabu kingine kilichochapishwa na tengenezo la Yehova chenye habari kama zinazopatikana kwenye vitabu hivyo, na kinachozungumzia mafundisho ya msingi ya Biblia na matakwa ya Mungu ya uadilifu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki