Matangazo
● Toleo la fasihi kwa Juni na Julai: Kuokolewa Kuingia katika Dunia Mpya au Furaha—Namna ya Kuipata. Agosti na Septemba: Kimoja cha broshua zifuatazo zenye kurasa 32 ukubwa wa gazeti: Furahia Maisha Milele Duniani!, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Serikali Itakayoleta Paradiso, au Mashahidi wa Yehova Katika Karne ya Ishirini. Oktoba: Andikisho la mwaka mmoja la ama Amkeni! ama Mnara au yote mawili.
● Akiba ya kutosha ya fomu zitakazotumiwa wakati wa mwaka wa utumishi wa 1989 zinapelekwa kwa kila kundi. Kwa kuwa kiasi kikubwa cha fedha kinatumiwa katika kuchapa na kupeleka, fomu hizo hazipasi kutumiwa vibaya. Zinapasa kutumiwa tu kwa kusudi linalonuiwa. Makundi mengine yamelazimika kuagiza fomu kabla ya mwisho wa utumishi wa mwaka kwa sababu nyingi zilitumiwa vibaya, kama vile kuandika habari. Makundi yanapasa kufanya mipango mingine kwa ajili ya karatasi za kuandikia.
● Kuanzia Septemba, waangalizi wasafirio watatoa hotuba ya watu wote “Kuvumilia Katika Kazi Njema Kunaleta Thawabu.” Hotuba ya watu wote itakayotolewa na waangalizi wa wilaya kuhusiana na mfululizo mpya wa makusanyiko ya mzunguko yanayoanza katika Septemba itakuwa “Kwa Nini Kuogopa Mungu wa Kweli?”
● Mafunzo ya Kitabu ya Kundi yataanza kujifunza kitabu “Wenye Umoja Katika Ibada ya Mungu wa Pekee wa Kweli” wakati wa juma la Agosti 15, 1988.
● Makundi ya Kenya tafadhali angalieni bei mpya ya Biblia ya kawaida ya Kiswahili ni 60/= kundi na watu wote. Bei ya mapainia inabaki kuwa 45/=.