Matangazo
● Toleo la fasihi kwa ajili ya Februari: Chochote cha vitabu vya kurasa 192 kilichochapishwa kabla ya 1980 ambacho kundi inacho akibani kwa nusu ya mchango wa kawaida, isipokuwa vifuatavyo: Maisha ya Jamaa, Mwalimu Mkuu, Uzima Ndio Uu Huu, Kweli, na Ujana. (Kuhusu kuchukua kwa deni, wazee wapaswa kurejeza kwenye miongozo katika Huduma ya Ufalme ya Desemba 1988). Ikiwa kundi halina akiba ya vitabu vya kutolewa kwa nusu ya mchango wa kawaida, kitabu Usalama Ulimwenguni Pote chapasa kutolewa kwa mchango wa kawaida. Machi: The Bible—God’s Word or Man’s? Aprili na Mei: Uandikisho wa Mnara wa Mlinzi. Mahali pasipopatikana uandikisho, magazeti mawili na nakala ya broshua yoyote, vyaweza kutolewa isipokuwa broshua Shule.
● Mwandishi na mwangalizi wa utumishi wapaswa kupitia utendaji wa mapainia wa kawaida wote. Ikiwa kuna wowote wanaotatizika kutimiza takwa la saa, wazee wapaswa kupanga msaada utolewe. Kwa ajili ya madokezo, pitieni barua za Sosaiti (S-201) ya Oktoba 1, 1988, na Oktoba 1, 1989. Pia, angalieni mafungu 12-20 ya nyongeza ya Huduma ya Ufalme Yetu ya Septemba 1986.
● Sherehe ya Ukumbusho itafanywa Jumanne, Aprili 10, 1990. Ingawa hotuba yaweza kuanza mapema, tafadhali kumbukeni kwamba kupitishwa kwa mkate na divai ya Ukumbusho hakupasi kuanza mpaka baada ya jua kutua. Chunguzeni kwenye vyanzo vya mahali penu mjue ni wakati gani jua linashuka mahali penu. Hakuna mikutano mingine inapasa kuongozwa tarehe hiyo. Ikiwa kwa kawaida kundi lenu linakuwa na mikutano Jumanne, huenda mngependa kuihamisha mpaka wakati mwingine wa juma ikiwa jumba linapatikana. Ikiwa Mkutano wa Utumishi wenu unaathiriwa, huenda ikawezekana kuunganisha na Mkutano wa Utumishi mwingine sehemu zozote zilizoratibiwa kwa ajili ya juma hilo ambazo ni zenye manufaa mahususi kwa kundi lenu.
● Gazeti Amkeni! la Kiarabu lilikuwa kichapo cha mara mbili kila mwezi kuanzia na toleo la Januari 8, 1990.
● Vichapo vinavyotazamiwa katika akiba karibuni:
Kiongozi cha Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Je! Uzima Ndio Uu Huu Tu?
Kumsikiliza Mwalimu Mkuu
“Habari Njema Hizi za Ufalme”
Wenye Umoja Katika Ibada ya Mungu wa Pekee wa Kweli
Kuokolewa Kuingia Katika Dunia Mpya
Kupata Faida Zote za Ujana Wako