Matangazo
● Toleo la fasihi la Februari: Kitabu chochote cha kurasa 192 kilichochapwa kabla ya 1980 ambacho kundi linacho akibani kwa nusu ya bei ya kawaida. (Kuhusu kuomba kupunguziwa deni, wazee wapaswa kurejezea mwongozo katika Huduma ya Ufalme Yetu ya Desemba 1988, ukurasa wa 3.) Ikiwa kundi halina vitabu hivyo akibani, kitabu Kuokolewa Kuingia Katika Dunia Mpya kitolewe kwa bei ya kawaida. Kitabu Kuokolewa chaweza kuagizwa kutoka kwa ofisi ya tawi. Machi: Kitabu Upeo wa Ufunuo. Aprili na Mei: Uandikishaji wa Mnara wa Mlinzi.
● Mwandishi pamoja na mwangalizi wa utumishi wapaswa kupitia utendaji wa mapainia wote wa kawaida. Ikiwa wowote wana magumu ya kufikia takwa la saa, wazee wapaswa kupanga usaidizi utolewe. Ili kupata madokezo, pitieni barua za Sosaiti (S-201-SW) za Oktoba 1, 1989, na Oktoba 1, 1990. Pia angalieni mafungu 12-20 ya nyongeza ya Huduma ya Ufalme Yetu ya Septemba 1986.
● Kuhusu utumishi wa painia, vikumbusho vifuatavyo vinatolewa:
○ Tangazo lapasa kutolewa kundini wakati painia wa kawaida aachapo utumishi wa painia. Tangazo hilo fupi laweza kutaarifu tu: “Hii ni kujulisha kundi kwamba [jina] hatumikii tena akiwa painia wa kawaida.”
○ Takwa la saa kwa mapainia wa kawaida lingali saa 1,000.
○ Mwaka mzima lazima uwe umepita baada ya karipio la halmashauri ya hukumu au kurudishwa kundini kwa mtu aliyetengwa kabla mtu huyo hajafikiriwa kwa utumishi wa painia msaidizi au wa kawaida.—Ona nyongeza ya Huduma ya Ufalme Yetu, Septemba 1986, mafungu 21 na 23.
● Painia yeyote wa kawaida anayependezwa na kutumikia akiwa painia wa pekee wa muda katika eneo lililo pekee wakati wa kampeni ya Julai-Septemba wapaswa kutoa ombi lao kwa kuandikia ofisi ya tawi kabla ya Aprili 1, 1991. Chini ya barua hiyo tungethamini kupata maelezo mafupi kutoka kwa halmashauri ya utumishi ya kundi juu ya kupatikana na uwezekano mbalimbali wa painia huyo.
● Ukumbusho utaadhimishwa Jumamosi, Machi 30, 1991. Ijapokuwa hotuba yaweza kuanza mapema kidogo, tafadhali kumbukeni kwamba kupitishwa kwa mkate na divai ya Ukumbusho hakupasi kuanza mpaka baada ya jua kushuka. Pateni habari kutoka vyanzo vya kwenu ili kujua wakati wa jua kushuka katika eneo lenu. Hakuna mikutano mingine isipokuwa mikutano kwa ajili ya utumishi wa shambani itaongozwa tarehe hiyo. Ikiwezekana, makundi yaliyo na mikutano ya kawaida iliyoratibiwa siku hiyo wapaswa kupanga wawe na mikutano hiyo katika siku nyingine. Hakutakuwa na badiliko katika mikutano iliyoratibiwa Jumapili.
● Wahubiri wanaotaka kufanya utumishi wa painia msaidizi katika Machi na Aprili wapaswa kufanya mipango yao sasa na kutoa fomu zao za maombi mapema. Hiyo itasaidia wazee wafanye mipango inayohitajiwa ya utumishi wa shambani na kuwa na fasihi ya kutosha
● Vipya Vinavyopatikana Akibani:
Je! Uamini Utatu?—Kiswahili
Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!—Kiswahili
● Sosaiti imetoa broshua mpya katika Kiingereza kwa kusudi la pekee la kusaidia watu wa malezi ya Kihindu waelewe kweli. Jina layo ni Our Problems—Who Will Help Us Solve Them? (Matatizo Yetu—Nani Atatusaidia Tuyatatue?) Makundi yaliyo na watu wasemao Kiingereza wa malezi ya Kihindu katika eneo lao waweza kuagiza kiasi KIDOGO cha broshua hiyo. Ipatikanapo katika lugha nyingine, tangazo litatolewa.