Matangazo
◼ Toleo la fasihi kwa Oktoba: Uandikishaji wa Amkeni! au Mnara wa Mlinzi au magazeti yote mawili. Uandikisho usipopatikana, magazeti mawili na nakala ya broshua yoyote (isipokuwa broshua Shule) yaweza kutolewa kwa mchango wa kawaida. Novemba: Biblia New World Translation pamoja na kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu? Desemba: Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Januari: Kitabu chochote cha kurasa 192 kilichotangazwa katika 1980 au mapema zaidi. Ikiwa kundi halina akiba ya vitabu hivyo vya kuweza kutolewa, kitabu Amani na Usalama wa Kweli—Wewe Unaweza Kuupataje? kitolewe na chaweza kuagizwa kutoka kwa ofisi ya tawi au depo mbalimbali. Februari: Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. ANGALIA: Makundi ambayo bado hayajaagiza vifaa vya kampeni vilivyotajwa juu yapaswa yafanye hivyo kwenye Fomu ya Agizo la Vitabu (S-14-SW) ya kila mwezi itakayofuata.
◼ Makundi yapaswa yaanze kuagiza Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—1993 pamoja na agizo lao la fasihi la Oktoba. Vijitabu hivyo vitapatikana katika Kiamhari, Kiarabu, Kifaransa, Kiingereza, Kinyarwanda, na Kiswahili. Vijitabu Kuyachunguza Maandiko Kila Siku ni bidhaa za kuagizwa kwa kiasi.
◼ Kuanzia Januari 8, 1993, Amkeni! la Kiswahili litakuwa chapa sawia na la Kiingereza la mara mbili kila mwezi. Makundi yatataka kurekebisha agizo lao ifaavyo.
◼ Kadi za beji za mkusanyiko wa wilaya wa 1992 zitatiwa ndani pamoja na safirisho la fasihi. Hazitahitaji kuagizwa. Kulingana na ukubwa wa kila kundi, kadi hizo zitasafirishwa kwa vifungu vya 25. Ikiwa kadi za beji zaidi zinahitajiwa na kundi, hizo zapaswa ziagizwe katika Fomu ya Agizo la Vitabu (S-14-SW). Mwahitaji kuagiza vishikizo vya plastiki vya kadi za beji kwa wowote kundini wanaovitaka.
◼ Wote watanufaika kikamili zaidi kutokana na drama ya wakati barabara kwenye “Wachukuaji Nuru” Mkusanyiko wa Wilaya kwa kusoma usimulizi wa kihistoria uliopuliziwa roho uliorekodiwa kwenye 2 Wafalme 22:1–23:23 na 2 Mambo ya Nyakati 34:1–35:19 kabla ya kuhudhuria mkusanyiko.
◼ Kwa kuwa mkusanyiko mwaka huu utakuwa wa siku tatu, hakutakuwa na uhitaji wa kutofanya Funzo la Kitabu la Kundi katika juma la mkusanyiko.
◼ Ni jambo la maana kwa wahubiri mmoja mmoja na vikundi vya familia kufanya mipango hususa ya kushiriki kwa ukawaida katika utumishi wa shambani wakati wa kipindi cha mkusanyiko na miezi ya likizo. Ikiwa utakuwa mbali na kundi lako la nyumbani mwishoni mwa mwezi, hakikisha kupeleka ripoti yako ya utumishi wa shambani kwa mwandishi wa kundi kwa wakati unaofaa ili itiwe ndani pamoja na ripoti ya kundi ya mwezi huo.