Matangazo
◼ Toleo la fasihi kwa Februari: Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. Machi: Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu! Aprili na Mei: Uandikishaji wa Mnara wa Mlinzi. ANGALIA: Makundi yatakayohitaji vifaa vya kampeni vilivyotajwa juu yapaswa yaviagize kwenye Fomu ya Agizo la Vitabu (S-14-SW) ya mwezi utakaofuata.
◼ Mwandishi na mwangalizi wa utumishi wapaswa kupitia utendaji wa mapainia wote wa kawaida. Ikiwa wowote wana magumu ya kufikia takwa la saa, wazee wapange msaada utolewe. Kwa madokezo, pitieni barua za Sosaiti (S-201-SW) za Oktoba 1, 1992, na Oktoba 1, 1991. Pia, angalieni mafungu 12-20 ya nyongeza ya Huduma ya Ufalme Yetu ya Septemba 1986.
◼ Ukumbusho utaadhimishwa Jumanne, Aprili 6, 1993. Ingawa hotuba yaweza kuanza mapema kidogo, tafadhali kumbukeni kwamba kupitishwa kwa mkate na divai ya Ukumbusho hakupasi kuanza mpaka baada ya jua kushuka. Pateni habari kutoka vyanzo vya kwenu ili kujua wakati wa jua kushuka katika eneo lenu. Hakuna mikutano mingine isipokuwa mikutano kwa ajili ya utumishi wa shambani itaongozwa tarehe hiyo. Ikiwa kundi lenu kwa kawaida huwa na mikutano Jumanne, huenda mkataka kuibadilisha hadi wakati mwingine wa juma hilo ikiwa Jumba la Ufalme litapatikana. Ikiwa Mkutano wa Utumishi wenu unaathiriwa, huenda ikawezekana kutia pamoja katika Mkutano wa Utumishi mwingineo sehemu zozote zilizopangiwa juma hilo zinazotumika hasa kwa kundi lenu. Makundi yenye ziara ya mwangalizi wa mzunguko yapaswa yapange upya mikutano inayofanywa Jumanne jioni kwa kawaida.
◼ Wahubiri wanaotaka kufanya upainia msaidizi katika Machi na Aprili wapaswa kufanya mipango yao sasa na kutoa fomu zao za maombi mapema. Hiyo itasaidia wazee wafanye mipango inayohitajiwa ya utumishi wa shambani na kuwa na fasihi ya kutosha.
◼ Mapainia wa kawaida wanaopendezwa kushiriki katika kampeini ya mwaka huu ya maeneo ya mbali kuanzia Julai hadi Septemba wakiwa mapainia wa pekee wa muda waweza sasa kutoa maombi yao kupitia baraza la wazee (au halmashauri ya utumishi) la kundi lao, litakalotuletea maombi na mapendekezo yalo kwetu kufikia Aprili 15, 1993, hiyo ikiwa ni tarehe ya mwisho.
◼ Makundi yaweza kujifunza Mnara wa Mlinzi la Machi 15, 1993 kulingana na tarehe zilizochapwa katika gazeti hilo au upesi iwezekanavyo baada ya hapo. Hata hivyo, Huduma ya Ufalme Yetu itaendelea kuchapisha ratiba isiyokatizwa.
◼ Tafadhali kumbukeni kwamba funzo jipya la Biblia nyumbani laweza kuripotiwa baada ya kuongozwa mara mbili kufuatia ziara ambayo mpango wa funzo ulionyeshwa na kuna sababu ya kuamini kwamba funzo hilo litaendelea.
◼ Tunawafahamisha kwamba tuna vichapo mbalimbali akibani katika lugha zifuatazo: Kigujarati, Kihindi, Kipunjabi, na Kiurdu.
◼ Vichapo Vinavyopatikana Sasa:
Kifaransa: Kalenda ya 1993. Kiingereza: Buku la Mnara wa Mlinzi la 1985; Faharisi 1986-90; Kuyachunguza Maandiko Kila Siku 1993; broshua, Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?; Faraja kwa Walioshuka Moyo (Trakti Na. 20); Furahia Maisha ya Familia (Trakti Na. 21); Ni Nani Hasa Anayeutawala Ulimwengu? (Trakti Na. 22). Kiswahili: Faraja kwa Walioshuka Moyo (Trakti Na. 20); Furahia Maisha ya Familia (Trakti Na. 21); Ni Nani Hasa Anayeutawala Ulimwengu? (Trakti Na. 22).