Matanagazo
◼ Fasihi itakayotolewa Juni: Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Julai na Agosti: Yoyote ya broshua zifuatazo zaweza kutumiwa: Je! Kweli Mungu Anatujali?, Furahia Milele Maisha Duniani!, “Tazama! Mimi Nafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya,” Je! Uamini Utatu?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, au Serikali Itakayoleta Paradiso. Septemba: Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. TAARIFA: Makundi yatakayohitaji vifaa vya kampeni vilivyotajwa juu yapaswa yaviagize kwenye fomu ya Agizo la Vitabu (S-14-SW) la kila mwezi litakalofuata.
◼ Mwangalizi msimamizi au mtu aliyeagizwa naye anapaswa akague hesabu za kundi Juni 1 au upesi iwezekanavyo baada ya hapo. Toleeni kundi tangazo jambo hilo lifanywapo.
◼ Kuanzia Juni 21 habari ya funzo la kitabu itatolewa kutoka broshua, Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli?. Kwa kuwa hakuna maswali yameandaliwa pamoja na kichapo hicho, kila kiongozi wa funzo la kitabu atatayarisha maswali yanayofaa ya kukazia mambo makuu ya kila fungu. Kama ilivyo kawaida twatia moyo usomaji wa maandiko yaliyowekwa bila manukuu lakini si yale yaliyonukuliwa.