Matangazo
◼ Toleo la fasihi kwa Januari: Kitabu chochote cha kurasa 192 kilichochapwa kwenye karatasi inayobadili rangi na kuwa manjano au inayochakaa au chochote kilichotangazwa kabla ya 1980. Makutaniko ambayo hayana ugavi wa vitabu hivyo yaweza kutoa kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu. Februari: Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. Machi: Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu! Aprili na Mei: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni!, pia na broshua (isipokuwa broshua Shule). Mahali kupendezwa kunapatikana katika ziara za kurudia, maandikisho yaweza kutolewa. ANGALIA: Makutaniko yatakayohitaji vifaa vya kampeni vilivyotajwa juu yapaswa yaviagize kwenye Agizo la Fasihi (S-14-SW) ya kila mwezi itakayofuata. Vichapo vya zamani zaidi vya kampeni ya Januari vyapatikana katika ofisi ya tawi au depo mbalimbali, lakini makutaniko yapaswa kutumia vile yalivyo navyo tayari akibani.
◼ Makutaniko yapaswa kufanya mipango ifaayo kwa ajili ya Ukumbusho, ambao utaadhimishwa mwaka huu Jumamosi, Machi 26, baada ya jua kutua. Ingawa ni vizuri kwa kila kutaniko kuwa na Ukumbusho wao wenyewe, jambo hilo huenda lisiwezekane sikuzote. Mahali ambapo makutaniko kadhaa hutumia Jumba la Ufalme moja, huenda ikawa vema kwa kutaniko moja au zaidi kupata mahali pengine jioni hiyo. Ukumbusho haupaswi kuanza kuchelewa mno hivi kwamba watu wapya wenye kupendezwa wapate ugumu wa kuhudhuria. Zaidi ya hilo, mikutano hiyo isiwekewe wakati karibu-karibu hivi kwamba hakuna wakati wa kabla au baada ya sherehe wa kusalimia wageni, wa kufanya mipango ya kuendeleza msaada wa kiroho kwa wengine, au kwa ajili ya kujengana na kutiana moyo miongoni mwa waliopo. Baada ya kushughulikia mambo yote kikamili, wazee wapaswa kuangalia ni mipango gani itakayosaidia kwa kufaa wote watakaohudhuria Ukumbusho ili wanufaike kikamili kutokana na pindi hiyo.
◼ Kuanzia Februari, na si baada ya Machi 6, hotuba mpya ya watu wote kwa waangalizi wa mzunguko itakuwa “Kuugua kwa Viumbe vya Kibinadamu—Kutakoma Lini?”
◼ Hotuba ya pekee kwa ajili ya majira ya Ukumbusho wa 1994 itatolewa ulimwenguni pote Jumapili, Aprili 10. Kichwa cha hotuba hiyo kitakuwa “Je! Dini Inatamausha Jamii ya Kibinadamu?” Muhtasari wa hotuba utapeanwa. Makutaniko yatakayokuwa na ziara ya mwangalizi wa mzunguko, kusanyiko la mzunguko, au siku ya kusanyiko la pekee mwisho-juma huo watakuwa na hotuba ya pekee juma linalofuata. Hakuna kutaniko linalopaswa kuwa na hotuba ya pekee kabla ya Aprili 10.
◼ Vichapo Vipya Vinavyopatikana:
Kiamhari: Mashahidi wa Yehova—Wanafanya Mapenzi ya Mungu kwa Umoja Ulimwenguni Pote. Kiingereza: Watch Tower Publications Index 1991-1992.
◼ Sosaiti sasa inatokeza mabuku yaliyojalidiwa ya Kiingereza ya Mnara wa Mlinzi kwa miaka 1960 hadi 1969 vikiwa vifaa vya daima. Yeyote anayependezwa kupata mabuku hayo yaliyojalidiwa apaswa kuyaagiza kupitia kutaniko. Tafadhali kumbuka kwamba mabuku yaliyojalidiwa ni vifaa vya kuagizwa kipekee.