Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/94 uku. 7
  • Linda Dhidi ya Fadhili Itumiwayo Vibaya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Linda Dhidi ya Fadhili Itumiwayo Vibaya
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Habari Zinazolingana
  • Fanya Zaidi ya Kusema Tu: ‘Ukaote Moto na Kushiba’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Wazee Wanaosimamia Vema
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • “Mwendelee Kuwachukua Watu wa Namna Hiyo Kuwa Wapendwa Wanaothaminika”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Jinsi Ambavyo Kutaniko Limepangwa
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1994
km 2/94 uku. 7

Linda Dhidi ya Fadhili Itumiwayo Vibaya

1 Watu wa Yehova wajulikana kwa roho yao ya fadhili na ukarimu. Mara nyingi hiyo hujionyesha yenyewe kwa njia ya kimwili tunapoiga yule Msamaria mwenye ujirani ambaye Yesu alisema juu yake katika kielelezo chake chenye kugusa moyo. (Luka 10:29-37) Lakini, watu fulani ambao hawastahili msaada wa kimwili huenda wakajitahidi kuichukulia vibaya fadhili yetu. Hivyo, upendo wetu kwa wengine lazima usawazike kwa “hekima na ufahamu wote.”—Flp. 1:9.

2 Ndani ya Kutaniko: Kwa mfano, mtu anaweza kusema kwamba hana kazi au atoe sababu nyingine za kuomba msaada. Wakati mwingine watu hao hawatafuti kazi bali hutaka tu wengine wawaandalie mahitaji ya kimwili. Juu ya watu kama hao mtume Paulo aliamuru hivi: “Ikiwa mtu hataki kufanya kazi, basi, asile chakula.”—2 The. 3:10.

3 “Wakati na tukio lisilotazamiwa” hutupata sisi sote, kwa hivyo tukiwa na uhitaji wa vitu vya kimwili, tukikosa “riziki yetu,” hatupaswi kuhangaika kupita kiasi, kwa kuwa Yehova huandalia wale wanaompenda na wafanyao mapenzi yake. (Mhu. 9:11, NW; Mt. 6:11, 31, 32) Mwenye uhitaji huenda akaona kuna manufaa ya kuongea na mmoja wa wazee. Wazee huenda wakajua programu za serikali zilizowekwa kuandaa msaada na huenda ikawa wanaweza kusaidia kujaza karatasi zinazohitajiwa au wakaelewa matakwa ya programu kama hizo. Kwa tukio lolote lile, baraza la wazee linaweza kuchunguza hali ya kila mmoja anayeomba msaada na kufikiria jambo la kufanya.—Linganisha 1 Timotheo 5:3-16.

4 Wadanganyaji Wenye Kusafiri: Sosaiti inaendelea kupata ripoti kwamba watu fulani katika kutaniko wamekuwa wakipunjwa pesa na vitu vya kimwili na wadanganyaji wenye kusafiri. Hilo halipaswi kutushangaza, kwa kuwa Maandiko yaonya kwamba “watu wabaya na wadanganyaji wataendelea, na kuzidi kuwa waovu, wakidanganya na kudanganyika.” (2 Tim. 3:13) Mara nyingi wadanganyaji hao hudai kuwa wana shida na wanahitaji pesa ili wapate usafiri na chakula wakirudi nyumbani. Ijapokuwa wanaweza kusikika kuwa wenye moyo mweupe, katika visa vingi wao si Mashahidi wa Yehova kamwe bali wanasingizia tu kuwa hivyo.

5 Mtu mgeni akitaka msaada, ni jambo la hekima kumjulisha mmoja wa wazee wa kutaniko, ambaye anaweza kuongoza kwa kujua kama mtu huyo ni ndugu yetu. Kwa kawaida simu yapasa kupigwa kwa mmoja wa wazee wa kutaniko ili msimamo wa mtu huyo ujulikane. Ndugu na dada wa kweli ambao wanajipata wakiwa na uhitaji usiotazamiwa wataelewa kwamba aina hii ya kuulizia habari inafanywa ili kulinda wote wahusikao. Kwa upande ule mwingine, wadanganyaji wataonyeshwa wazi na aina hii ya uchanganuzi. Hakuna haja ya kuwa wenye kuwashuku kupita kiasi wote tusiowajua, lakini twapaswa kujilinda na wadanganyaji waovu.

6 Mfalme mwenye hekima Sulemani alishauri: “Usiwanyime watu mema yaliyo haki yao, ikiwa katika uwezo wa mkono wako kuyatenda.” (Mit. 3:27) Kwa kutumia utambuzi wetu wenye hekima, twaweza kuendelea kuwa wenye rehema huku tukilinda dhidi ya fadhili itumiwayo vibaya.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki