Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 3/94 uku. 1
  • Wafanye Wahisi Wamekaribishwa Kwenye Ukumbusho

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wafanye Wahisi Wamekaribishwa Kwenye Ukumbusho
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Habari Zinazolingana
  • Kuwasaidia Wote Ambao Wameonyesha Kupendezwa
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Wakaribishe Kwa Uchangamfu!
    Huduma ya Ufalme—2013
  • Tunaweza Kuwasaidiaje Watakaohudhuria Ukumbusho?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Ushahidi Mkubwa Utatolewa
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1994
km 3/94 uku. 1

Wafanye Wahisi Wamekaribishwa Kwenye Ukumbusho

1 Katika miaka michache iliyopita, ni mtu 1 kati ya watu 3 waliohudhuria Ukumbusho aliyekuwa mhubiri wa habari njema. Inawezekana kuwe hivyo pia mwaka huu. Baadhi yao huenda wakahudhuria kwa sababu ya kutiwa moyo kwa bidii na mtu wa ukoo au rafiki anayeishi katika jiji jingine, ilihali huenda ikawa wengine walikaribishwa na wahubiri wa huko. Na wengine wanaohudhuria, ijapokuwa wamebatizwa, si watendaji katika huduma. Twakaribisha kwa moyo mweupe wote wanaoheshimu amri hii ya Yesu: “Fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.”—1 Kor. 11:24; Rum. 15:7.

2 Wakaribishaji waliopewa mgawo huo wapaswa kuwa macho ili wakaribishe kila mtu, hasa mgeni, anapofika kwenye Jumba la Ufalme. Hata hivyo, sisi sote twaweza kushiriki kuonyesha ukaribishaji-wageni kwenye Ukumbusho. (Rum. 12:13) Twaweza kufanyaje hivyo?

3 Jioni hiyo wahubiri kadhaa watakuwa na shughuli nyingi ya kuandaa usafiri kwa watu wenye kupendezwa. Watu fulani huenda wakaweza kufika mapema na kuwapo ili kuwasalimu wageni wanaokuja wenyewe. Mgeni anapoingia kwenye jumba, msalimu kwa uchangamfu, na uanzishe mazungumzo. Muulize kama anajua mtu yeyote katika kutaniko lenu. Ikiwa anajua, mshughulikie hadi mtu huyo afike. (Linganisha Luka 10:35.) Ikiwa hajui mtu yeyote binafsi, kwa nini usimkaribishe akae na wewe wakati wa mkutano? Eleza jinsi divai na mkate utakavyotumiwa wakati wa programu. Huenda akahitaji msaada wako kuangalia maandiko yanayonukuliwa na msemaji.

4 Kwenye umalizio wa mwadhimisho wa Ukumbusho, mjulishe kuwa umefurahi kwamba amekuja. Huenda akawa na maswali juu ya kazi yetu ambayo waweza kujibu. Kupendezwa kwako kibinafsi kwaweza kuongoza kwenye mazungumzo juu ya habari fulani katika Biblia, iwe ni katika Jumba la Ufalme au kwingineko. Baadhi ya mafunzo mazuri zaidi yameanzishwa na ndugu walio macho ambao wamechukua hatua hii inayostahili pongezi. Kabla hajaondoka kwenye Jumba la Ufalme, mjulishe kwa wengine, na umkaribishe kwa moyo mkunjufu arudi tena.

5 Inapendeza kama nini kukaribisha ndugu na dada zetu wapendwa ambao wamekuwa hawahudhurii mikutano kwa ukawaida au ambao wamekuwa hawatendi katika huduma kwa muda fulani! Badala ya kuuliza maswali juu ya kwa nini hawajahudhuria mikutano, onyesha tu shangwe yako ya kuwa nao wakati huo. Labda jambo fulani watakalosikia wakati wa hotuba ya Ukumbusho litawachochea wafikirie tena uhusiano wao wa wakfu kwa Yehova. Ukaribishaji wako mchangamfu na hangaiko la kweli unaloonyesha laweza kugusa mioyo yao. Wajulishe kwamba unatazamia kuwaona tena.—Rum. 1:11, 12.

6 Hotuba ya pekee yenye kichwa “Dini ya Kweli Hutimiza Mahitaji ya Jamii ya Kibinadamu” itatolewa katika makutaniko karibu yote mnamo Aprili 10. Hakikisha kwamba wale wote wanaohudhuria mwadhimisho wa Ukumbusho wanakaribishwa na wanasaidiwa wawepo wakati huo. Ni tumaini letu kwamba wale wanaohudhuria mikutano hii ya pekee watahisi wamekaribishwa na wajionee roho ya uchangamfu ya ushirika miongoni mwa watu wa Yehova.—Zab. 133:1.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki