Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 10/94 uku. 1
  • Sasa Ndio Wakati

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sasa Ndio Wakati
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Habari Zinazolingana
  • Kujiwekea Miradi ya Mwaka Mpya wa Utumishi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Ninaweza Kufikia Miradi Yangu Jinsi Gani?
    Amkeni!—2010
  • Tumia Miradi ya Kiroho ili Kumtukuza Muumba Wako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
  • 12 Malengo
    Amkeni!—2018
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1994
km 10/94 uku. 1

Sasa Ndio Wakati

1 Mtume Paulo alipoandika barua yake ya pili kwa Wakorintho, aliwakumbusha kwamba walikuwa wameazimia kufanya kazi njema ya msaada kwa niaba ya waamini wenzao katika Yerusalemu. Hata hivyo, mwaka ulikuwa umepita, nao bado walikuwa hawajamaliza kazi iliyokuwa imeanzishwa. Kwa hiyo yeye aliwasihi: “Endeleeni mkaimalize: mwe wenye nia ya kuikamilisha madhumuni hiyo kama mlivyoichagua.”—2 Kor. 8:11, The New English Bible.

2 Sisi sote tumejiwekea miradi, wakati mmoja au mwingine. Huenda ikawa tumeamua kuongeza ushiriki wetu katika huduma ya shambani, ili tuwajue ndugu zetu vizuri, tuwe na ustahili wa pendeleo la utumishi, au kushinda udhaifu fulani. Ijapokuwa tulianza tukiwa na makusudi yanayofaa, huenda ikawa hatukuendelea kufikia mradi wetu. Kabla ya kutambua hilo, huenda majuma, miezi, au hata miaka ilipita bila ya sisi kusonga hata kidogo. Je, huenda ikawa twahitaji kutumia shauri la ‘kuendelea tukamalize’ tulichoanza?

3 Kufikia Miradi Yetu: Ni rahisi kufanya azimio la kibinafsi lakini ni vigumu sana kulitimiza. Kukawia kwaweza kuzuia maendeleo yoyote. Twahitaji kuamua na kisha tuazimie kuendelea bila kukawia. Mpango wa kibinafsi ni muhimu. Ni jambo la maana kuweka kando wakati unaohitajiwa kufanya kazi hiyo na uhakikishe wakati huo unatumiwa kwa kusudi hilo. Ni wazo zuri kuweka tarehe ya mwisho na ujipe nidhamu kwa kuhakikisha kwamba tarehe hiyo imefikiwa.

4 Tunaposhindwa kufikia miradi yetu, ni rahisi kusababu: ‘Nitafanya baadaye.’ Lakini hatujui kitakachotokea wakati ujao. Mithali 27:1 husema: “Usijisifu kwa ajili ya kesho; kwa maana hujui yatakayozaliwa na siku moja.” Mwanafunzi Yakobo alionya dhidi ya kuwa mwenye uhakika mno juu ya wakati ujao kwa sababu “hamjui yatakayokuwako kesho. . . . Basi yeye ajuaye kutenda mema, wala hayatendi kwake huyo ni dhambi.”—Yak. 4:13-17.

5 Kukiwa na vikengeusha fikira vingi pamoja na madai yanayofanywa na wengine, miradi yetu yaweza kutatizwa. Jitihada yenye bidii yahitajiwa ili kuiweka wazi akilini. Kuweka jambo hilo katika sala zetu kwasaidia. Kuwaomba wengine tulio na ukaribu nao ili watukumbushe na kututia moyo kwaweza kufanyiza tofauti. Kutia alama katika kalenda yetu kutakuwa kikumbusha cha kuchunguza maendeleo yetu. Mtu apaswa kuamua “atende kama alivyokusudia moyoni mwake.”—2 Kor. 9:7.

6 Mwezi wa Oktoba watoa fursa nzuri ya kukazia fikira miradi yetu. Tutakuwa tukitoa uandikishaji wa Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Je, tungeweza kuweka miradi fulani yenye kufikika? Vipi juu ya kuongeza maangusho yetu ya magazeti? Kuamua kufanya ziara za kurudia zaidi na kuanzisha funzo la Biblia jipya yaweza kuwa miradi inayofaa kwa wengi.

7 Si jambo la hekima kuahirisha jambo la maana, kwa kuwa “dunia inapita.” (1 Yoh. 2:17) Mapendeleo na baraka za pekee katika utumishi wa Yehova zapatikana kwetu sasa. Inategemea sisi kuzitumia vizuri.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki