Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 3/95 uku. 4
  • Kupiga Mbiu ya ‘Maneno ya Unabii’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kupiga Mbiu ya ‘Maneno ya Unabii’
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Habari Zinazolingana
  • Tangaza Ujumbe Wenye Kusisimua Uliomo Katika Ufunuo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1994
  • Ufunuo—Mafumbo Yafumbuliwa
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Kutangaza Habari Njema Kwa Kutumia Toleo Jipya
    Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Kutoa Habari Njema kwa Hisi ya Uharaka
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1995
km 3/95 uku. 4

Kupiga Mbiu ya ‘Maneno ya Unabii’

1 Sisi tunaishi katika wakati ambapo unabii mwingi katika kitabu cha Ufunuo unatimizwa. Wengi wanatafuta kuelewa maana ya matukio yenye kuvuruga yanayotendeka. Wao wanaweza kunufaika kutokana na ‘kusikia maneno’ ya unabii wa Ufunuo. (Ufu. 1:3) Wakati wa mwezi wa Machi, tuna fursa ya kuwasaidia kwa kukazia kitabu Upeo wa Ufunuo. Tunapokitoa twapaswa kukumbuka kwamba matatizo yanayokabili wanadamu leo yalitabiriwa katika kitabu cha Ufunuo. Twaweza kusema nini basi?

2 Mfikio huu waweza kuwa wenye matokeo:

◼ “Vita, njaa, na ugonjwa umekumba wanadamu katika karne hii ya 20. Je, wewe wafikiri ni kwa nini ni hivyo hali mwanadamu amefanya maendeleo mengi sana ya kiufundi? [Ruhusu itikio.] Wengi wanashangaa kujua kwamba hali hizo zote zilitabiriwa katika Biblia. Yaelekea wafahamu usemi ‘wale wapanda-farasi wanne wa Apokalipsi.’ Kile Biblia husema juu ya wapanda-farasi hao kwa kweli ni unabii unaotimizwa katika matukio ya ulimwengu leo. [Fungua kitabu Upeo wa Ufunuo kwenye sura 16, na uonyeshe vielezi kwenye kurasa 91-97.] Ingawa unabii huu hutabiri juu ya wakati wa msononeko mkubwa, unatoa tumaini pia. [Soma Ufunuo 6:2 katika fungu 3.] Mpandaji wa farasi mweupe ni Yesu Kristo. Yeye ameahidi kushinda uovu na kuleta ulimwengu wenye furaha na amani kupitia ule Ufalme aliotufundisha tuombe.” Toa kitabu.

3 Labda swali hili laweza kuchochea mazungumzo yenye maana:

◼ “Wewe wahisi ni nini kihitajiwacho ili kuondoa hali mbaya ulimwenguni? [Ruhusu itikio.] Watu walio wengi hukubali kwamba kuna uhitaji wa mabadiliko makubwa ikiwa ulimwengu huu utaokoka. Biblia huonyesha kwamba Mungu ajua jinsi ya kusuluhisha matatizo yetu naye ameahidi kutusaidia.” Fungua kitabu Upeo wa Ufunuo, ukurasa 171, na usome Ufunuo 11:15 katika fungu 1. Fungua kwenye vielezi kwenye kurasa 302 na 308, na uonyeshe baraka zitakazotimia chini ya utawala wa Ufalme kupitia Kristo. Kisha ueleze jinsi mwenye nyumba binafsi awezavyo kunufaika.

4 Huenda ukahisi starehe kusema jambo fulani kama hili:

◼ “Watu wengi ambao wamesoma kitabu cha Biblia cha Ufunuo walikiona kuwa kigumu kuelewa. Chafafanua matukio mbalimbali yasiyo ya kawaida. Kitabu hiki, Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!, chaandaa maelezo ya mstari kwa mstari juu ya kitabu kizima cha Ufunuo na chaonyesha jinsi sisi binafsi tunavyoathiriwa na utimizo wa unabii wacho mwingi.” Fungua kitabu kwenye ukurasa 15, fungu 2, na uonyeshe Ufunuo 1:1 katika herufi nzito. Eleza kwamba maelezo hususa ya aina hiyo yanaandaliwa juu ya kila mstari katika kitabu cha Ufunuo na kwamba habari hii itamsaidia aelewe unabii huu mwingi ulio wenye kutokeza. Toa kitabu kwa njia yenye mtazamo chanya.

5 Ikiwa mtu ana shughuli nyingi au huna hakika kuna kupendezwa kwa kutosha, waweza kuacha gazeti au trakti. Unaporudi na kupendezwa kwaonyeshwa, kitabu kingeweza kutolewa.

6 Ujumbe uliomo katika Ufunuo waathiri wanadamu wote. Kila mtu ahitaji kusikia maneno ya unabii. Na tufanye yote tuwezavyo kupiga mbiu ya ujumbe huu muhimu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki