Matangazo
◼ Fasihi itakayotolewa wakati wa Machi: Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu! Aprili na Mei: Maandikisho ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Juni: Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation? TAARIFA: Makutaniko ambayo bado hayajaagiza vifaa vya kampeni vilivyotajwa juu yapaswa kufanya hivyo kwenye Agizo la Fasihi (S-14-SW) lao la kila mwezi litakalofuata.
◼ Mwangalizi-msimamizi au mtu yeyote aliyechaguliwa naye apaswa kukagua hesabu za kutaniko mnamo Machi 1 au upesi iwezekanavyo baada ya hapo. Tangazia kutaniko hilo lifanywapo.
◼ Mwandishi na ndugu anayeshughulika na hesabu za kutaniko wanaombwa kwa fadhili wahesabu kihalisi maombi ya kupunguziwa bei ya mapainia na kuorodhesha hayo kama vile iombwavyo kwenye fomu ya S-20-SW inayotumiwa sasa.