Habari Njema kwa Wanyenyekevu
1 Twaishi wakati wa hukumu inayokaribia. (Eze. 9:5, 6) Ni muhimu kwamba watu wanyenyekevu kila mahali wajulishwe ili kwamba wajitayarishe kwa ajili ya linalokuja. Kwa fadhili-upendo zake, Yehova ameagiza watu wake ‘wawahubiri wanyenyekevu habari njema.’ (Isa. 61:1, 2) Magazeti yetu hutusaidia tutangaze habari njema kila mahali.
2 Mnara wa Mlinzi na Amkeni! huandaa chakula cha kiroho ambacho hututia nguvu na kutuhamasisha. Mnara wa Mlinzi hufariji wanyenyekevu kwa habari njema kwamba Ufalme wa Mungu karibuni utaigeuza dunia kuwa paradiso. Amkeni! hujenga uhakika katika ahadi ya Muumba ya kuleta ulimwengu mpya wenye amani na usalama. Ugawanyaji wenye kuenea wa majarida haya ni mojapo njia za haraka zaidi za kuleta habari njema kwa wanyenyekevu. Ni mambo gani ya kuongea tuwezayo kukazia katika matoleo ya karibuni?
3 Unaweza kutoa “Mnara wa Mlinzi” kwa kuelekezea makala inayofaa na kuuliza swali:
◼ “Unafikiri twaweza kupata manufaa gani kwa kusoma Biblia? [Ruhusu itikio.] Biblia yenyewe, kwenye Warumi 15:4, hutusaidia tusababu juu ya swali hilo. [Soma Warumi 15:4.] Watu walio wengi katika jamii yetu wana Biblia, lakini wachache hupata wakati wa kuisoma kwa ukawaida. Twaamini kwamba tumaini hakika pekee la wakati ujao lapatikana katika Biblia, na tutabarikiwa tukiisoma.” Toa maelezo ya ziada yafaayo, kisha utoe maandikisho.
4 Ikiwa “Mnara wa Mlinzi” latoa makala inayozungumzia kifo unaweza kuamsha kupendezwa kwa utangulizi huu:
◼ “Mara nyingi watu wengi wamejiuliza vile mababu wao waliokufa walivyokuwa. Kwa kuwa wamekufa na hawapo tena, watu walio wengi hukata kauli kwamba hatutawaona tena kamwe. Je, wafikiri kuna uwezekano wowote kwamba tutapata kuwajua mababu wetu waliokufa?” Ruhusu itikio. Soma Yohana 5:28, 29, na ueleze jinsi Mungu ameahidi kuwapa uhai mpya katika dunia paradiso.
5 Unaweza kutoa “Amkeni!” kwa kuuliza swali hili:
◼ “Unafikiri ni nini kitakachohitajiwa ili kufanya maisha yastahili?” Ruhusu itikio. Rejezea kwenye makala inayofaa katika gazeti hilo na usome yale Sulemani alisema katika Mhubiri 2:11. Kisha, onyesha shauri lake kwenye sura 12, mstari 13. Mkaribishe mwenye nyumba akubali maandikisho au magazeti kwa mchango wa kawaida.
6 Ikiwa unatumia magazeti kabla ya Mei 14, hakikisha unabeba nakala za trakti Habari za Ufalme Na. 34 na kumtolea yeyote ambaye hajapokea nakala bado. Twapaswa sikuzote kuwa tayari kutoa fasihi yetu, tukitambua kwamba yaweza kusomwa na wengine katika familia na vilevile marafiki ambao huenda wakawatembelea. (1 Tim. 6:18) Habari njema tuleteazo wanyenyekevu zaweza kuokoa maisha zao.—1 Tim. 4:16.