Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 9/95 uku. 1
  • Kuchunguzwa na Yehova —Kwa Nini Kwanufaisha?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuchunguzwa na Yehova —Kwa Nini Kwanufaisha?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Habari Zinazolingana
  • Dumisha Imani na Afya Yako ya Kiroho
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Uwe na Maoni Yanayopatana na Maandiko Kuhusu Matibabu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Je, Wewe Hula Vyema Kiroho?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Unaweza Kuepuka Ugonjwa wa Moyo wa Mfano
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1995
km 9/95 uku. 1

Kuchunguzwa na Yehova —Kwa Nini Kwanufaisha?

1 Kila mtu hutamani afya nzuri. Yafanya maisha yawe yenye kufurahisha zaidi. Hata hivyo, wengi wanaofurahia afya nzuri bado hupata kuchunguzwa na daktari pindi kwa pindi. Kwa nini? Wanataka matatizo yoyote ya afya yanayositawi yapatikane ili hatua ziweze kuchukuliwa kuyaponya. Ni jambo la maana hata zaidi kulinda afya yetu ya kiroho. Kibali cha Yehova chategemea kuendelea kwetu kuwa “wenye afya katika imani.”—Tito 1:13, NW.

2 Huu ndio wakati ufaao wa kuchunguzwa na Yehova. Kwa nini? Kwa sababu Yehova yumo katika hekalu lake takatifu, naye anachunguza mioyo ya wanadamu wote. (Zab. 11:4, 5; Mit. 17:3) Kama vile Daudi, sisi humwomba Yehova atuchunguze kikamili: “Unichunguze, Ee Yehova, na kunitia kwenye jaribu; unisafishe figo zangu na moyo wangu.”—Zab. 26:2, NW.

3 Ni lazima tujilinde na matisho dhidi ya afya yetu ya kiroho ambayo huenda yakatoka ndani yetu kwa sababu ya mwili wetu usio mkamilifu. Mithali 4:23 yashauri hivi: “Linda moyo wako kuliko yote uyalindayo; maana ndiko zitokako chemchemi za uzima.”

4 Afya yetu ya kiroho yaweza kutishwa pia na ulimwengu mfisadi, usio wa adili, unaotuzunguka. Tukijiruhusu kuukaribia sana mfumo huu mbovu, tungeweza kuanza kufikiri kama vile unavyofikiri na kusitawisha mitazamo ya kilimwengu. Au huenda tukaamua kufuata mtindo-maisha wa kilimwengu kisha tukashindwa na roho ya ulimwengu.—Efe. 2:2, 3.

5 Shetani aweza kutumia mnyanyaso au upinzani wa moja kwa moja akijitahidi kutuangamiza kiroho. Hata hivyo, mara nyingi sana yeye hutumia kwa ujanja uvutio mbalimbali wa kilimwengu ili kutushawishi. Petro atuhimiza ‘tuwe na kiasi na kukesha,’ kwa kuwa Shetani ni kama ‘simba angurumaye, akitafuta mtu ammeze.’ Tunahimizwa ‘tumpinge tukiwa thabiti katika imani.’—1 Pet. 5:8, 9.

6 Kuna uhitaji wa kulinda afya yetu ya kiroho, kuweka imani yetu ikiwa thabiti kwa kuiimarisha kila siku. Mtume Paulo apendekeza kwamba tuijaribu imani yetu sikuzote. Kama vile tunavyotii kwa hekima shauri lenye kutumika tunalopewa na daktari mwenye uwezo, sisi humsikiliza Yehova pia wakati uchunguzi Wake wa kiroho ufunuapo tatizo linalohitaji kusahihishwa. Hilo lafanya iwezekane kwetu “kurekebishwa upya.”—2 Kor. 13:5, 11, NW.

7 Kwa kweli Yehova ndiye Mchunguzi mkuu. Upimaji wake ni sahihi sikuzote. Yeye hujua barabara kile tunachohitaji. Kupitia Neno lake na ‘mtumwa mwaminifu,’ yeye hupendekeza chakula cha kiroho chenye afya. (Mt. 24:45; 1 Tim. 4:6) Kula chakula cha kiroho chenye lishe kwa kawaida nyumbani na kwenye mikutano ya kutaniko kwatuwezesha tuendelee kuwa wenye afya kiroho. Mazoezi ya kiroho ya kawaida katika huduma na utendaji mwingine wa Kikristo yananufaisha pia. Kwa hiyo, sisi hukaribisha kuchunguzwa na Yehova kwa kawaida, tukiwa na uhakika kwamba yeye atatuweka tukiwa na afya bora zaidi ya kiroho.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki