Desemba Imefika Tena!
1 Wengi wetu twatazamia wakati wa sikukuu, tunapoweza kufurahia likizo yenye kustarehesha na wakati fulani pamoja na rafiki zetu. Hata hivyo, twahitaji kujikumbusha kwamba utendaji wa kitheokrasi lazima uendelee ukiwa wa kwanza kabisa katika orodha yetu ya mambo ya kutangulizwa. Bado twataka kushiriki kwa ukawaida katika utumishi wa shambani na kuhakikisha kwamba unaripotiwa bila kukawia katika kutaniko. Tukisafiri kwingineko, twapaswa kujaribu kuhudhuria mikutano ya kutaniko. Tukibeba fasihi kadhaa zifaazo, huenda tukaweza kutoa kitu fulani tunapokuwa na pindi ya kutoa ushahidi wa vivi hivi.
2 Vijana ambao hawako shuleni wanaweza kufikiria uwezekano wa kujiandikisha wawe mapainia-wasaidizi. Sisi sote twapaswa kujaribu kudumisha ratiba yetu ya funzo la kibinafsi, ambayo hutia ndani usomaji wa Biblia na habari ya kushughulikiwa kila juma kwenye mikutano. Tunapokubali badiliko katika kawaida yetu ya kila siku wakati wa hii sikukuu ya Desemba, bado twataka kuendelea na ‘mambo ya kiroho yaliyo ya maana zaidi.’—Flp. 1:10, NW.