Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/95 uku. 8
  • Rudia Wale Walioonyesha Kupendezwa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Rudia Wale Walioonyesha Kupendezwa
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1995
Huduma Yetu ya Ufalme—1995
km 12/95 uku. 8

Rudia Wale Walioonyesha Kupendezwa

1 Kwenye 1 Wakorintho 3:6, Paulo aliandika: “Mimi nilipanda, Apolo akatia maji; bali mwenye kukuza ni Mungu.” Paulo alitumia kusababu huku ili kusaidia ndugu zake kuona uhitaji wa kufanya kazi kwa muungano chini ya ukichwa wa Kristo. Kwa njia hii pia aliwasaidia wathamini sehemu muhimu waliyokuwa nayo katika kazi ya maana ya kupanda na kutia maji.

2 Kazi hiyo ya kuokoa uhai italetwa kwenye tamati siku hiihii. Tukiwa Wakristo walio wakfu, twashiriki daraka zito la kusaidia wengine wawe wafuasi wa Yesu. (Mdo. 13:48) Utafuatiaje kupendezwa ulikoweza kuamsha kwa kutumia kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi?

3 Ikiwa unarudi kuzuru mtu aliyekubali kitabu, waweza kusema:

◼ “Tulipoongea mara ya mwisho, tulizungumzia Yesu Kristo alikuwa mtu wa aina gani. Nilifurahi kukuachia kile kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Ni nini kimekupendeza zaidi kuhusu mafundisho ya Yesu na kuhusu utu wake?” Ruhusu itikio. Fungua sura ya 113, na uzungumzie kielelezo bora zaidi cha Yesu cha unyenyekevu. Soma Wafilipi 2:8 kuonyesha jinsi mtume Paulo aliona mwelekeo wa Yesu wa unyenyekevu. Kisha unaweza kueleza jinsi tunavyoweza kujifunza mengi zaidi kupitia funzo la kawaida la Biblia.

4 Huenda ukapendelea utangulizi huu:

◼ “Tuliongea kuhusu mambo aliyofanya Yesu alipokuwa duniani ambayo yaonyesha anatujali kwelikweli. Unafikiri atafanya nini mwishowe ili apumzishe wale ambao wameteseka sana?” Ruhusu itikio. Fungua ukurasa 133, na upitie maelezo yaliyo kwenye fungu la tano. Fungua kwenye picha iliyo katika ukurasa ufuatao, na ueleze kutakavyokuwa wakati mapenzi ya Mungu yafanywapo duniani kama yalivyo mbinguni. Taja manufaa zitakazopatikana kwa kujifunza mengi zaidi.

5 Au huenda ukataka kutumia mfikio huu wa moja kwa moja:

◼ “Mara ya mwisho nilipokuwa hapa, tulizungumzia umaana wa kupata ujuzi kuhusu Yesu. Yohana 17:3 husema kwamba ‘kwamaanisha uhai wa milele’ kutwaa ujuzi huo. Twaweza kufanyaje hivyo?” Ruhusu itikio. Endelea kwa kueleza mpango wetu wa kujifunza Biblia na jinsi ya kuutumia kwa manufaa.

6 Paulo asema kwamba mfanya kazi “atapata thawabu yake mwenyewe sawasawa na taabu yake mwenyewe” wakati wa mavuno. (1 Kor. 3:8) Tukijitahidi wenyewe kwa bidii katika kusaidia wengine wawe wafuasi wa Yesu, thawabu yetu itakuwa kubwa kwa hakika.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki