Matangazo
◼ Fasihi itakayotolewa wakati wa Januari: Kitabu chochote chenye kurasa 192 kilichotangazwa kabla ya 1982 ambacho kutaniko laweza kuwa nacho akibani, kwa nusu-bei kwa wahubiri na pia mapainia kwa nusu-bei ya painia. Makutaniko ambayo hayana akiba ya vitabu hivyo yaweza kutoa Kuokolewa Kuingia Katika Dunia Mpya. Februari: Kitabu Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha au Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu! Machi: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Aprili: Maandikisho ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mahali ambapo andikisho halichukuliwi toa magazeti yote mawili kwa mchango wa kawaida au broshua yoyote yaweza pia kutumiwa (isipokuwa broshua Elimu na Shule). TAARIFA: Makutaniko ambayo bado hayajaagiza vifaa vya kampeni vilivyotajwa juu yapaswa kufanya hivyo katika Fomu ya Kuomba Fasihi yao ya kila mwezi itakayofuata (S-14-SW).
◼ Makutaniko yapaswa kufanya mipango ifaayo ili kuadhimisha Ukumbusho mwaka huu Jumanne, Aprili 2, baada ya jua kushuka. Ijapokuwa inapendeza kwa kila kutaniko kuwa na mwadhimisho wake wenyewe wa Ukumbusho, huenda isiwezekane sikuzote. Mahali ambapo kwa kawaida makutaniko kadhaa hutumia Jumba la Ufalme lilelile, labda kutaniko moja au mawili yaweza kujipatia utumizi wa jengo jingine jioni hiyo. Ukumbusho haupaswi kuanza ukichelewa mno hivi kwamba watu wapya wanaopendezwa waone ugumu wa kuhudhuria. Zaidi ya hayo, ratiba haipaswi kuwa yenye shughuli nyingi sana hivi kwamba hakuna wakati wa kusalimia wageni kabla na baada ya mwadhimisho, kufanya mipango ya usaidizi wa kiroho wenye kuendelea kwa wengine, au kufurahia badilishano la ujumla la kitia-moyo. Baada ya kufikiria kikamili mambo yote, wazee wapaswa kuamua ni mipango gani itakayosaidia vizuri zaidi wale wanaohudhuria Ukumbusho ili wanufaike kikamili kutokana na pindi hiyo.
◼ Hotuba ya pekee ya majira ya Ukumbusho ya 1996 itatolewa Jumapili, Aprili 21. Kichwa cha hotuba hiyo kitakuwa “Kudumu Bila Mawaa Kati ya Kizazi Kilichopotoka.” Muhtasari utaandaliwa. Makutaniko yatakayokuwa na ziara ya mwangalizi wa mzunguko, kusanyiko la mzunguko, au siku ya kusanyiko la pekee mwisho-juma huo yatakuwa na hotuba ya pekee juma litakalofuata. Hakuna kutaniko lipaswalo kuwa na hotuba ya pekee kabla ya Aprili 21.
◼ Kuanzia Februari, na si baada ya Machi 3, hotuba mpya ya watu wote ya waangalizi wa mzunguko itakuwa “Kutaniko Lenye Uaminifu-Mshikamanifu Chini ya Uongozi wa Kristo” au wonyesho wa slaidi “Ufundishaji wa Kimungu Hushinda Ulimwenguni Pote” katika mizunguko ambayo haijaona wonyesho huu wa slaidi.