Matangazo
◼ Toleo la fasihi kwa Agosti: Yoyote ya broshua zenye kurasa 32 zifuatazo: Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je! Uamini Utatu?, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?, Serikali Itakayoleta Paradiso, na “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya.” Mahali panapofaa, broshua kama vile Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?, Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli?, na Our Problems—Who Will Help Us Solve Them? zaweza kutolewa. Inadokezwa kwamba kitabu Kuishi Milele kitolewe tunapohubiri eneo lililo pekee na lisilohubiriwa mara nyingi. Septemba: Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha. Makutaniko yaliyo na vitabu vya Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani, au Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation? akibani, hivi vyaweza kutolewa. Oktoba: Maandikisho ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mahali ambapo andikisho halikubaliwi, toa magazeti yote mawili kwa mchango wa kawaida. Novemba: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Jitihada ya pekee itafanywa kufuatia maangusho yote, tukiwa na kusudi la kuanzisha mafunzo ya Biblia nyumbani.
◼ Tafadhali ona kwamba tarehe za mkusanyiko wa wilaya wa Nairobi zimebadilishwa hadi Desemba 27-29, 1996. Mkusanyiko wa eneo la Mt. Kenya utafanywa Nyeri bila kubadili tarehe, yaani, Desemba 27-29, 1996.
◼ Matembezi kwenye ujenzi wa jengo jipya la tawi yanawezekana Jumatano hadi Jumapili kati ya saa 2:00 asubuhi hadi saa 6:00 na saa 7:00 hadi saa 11:00 alasiri. Itakuwa vizuri ukija na kadi yako ya Mwelekezo wa Mapema Kuhusu Tiba/Ondoleo la Hatia.
◼ Watangazaji wanaopanga kuanza utumishi wa painia wa kawaida Septemba 1, 1996 wapaswa kutoa ombi bila kuchelewa.
◼ Mwandishi wa kutaniko atakusanya ripoti za utumishi kwa ajili ya kuingiza kwenye fomu ya Ripoti ya Mchanganuo wa Kutaniko (S-10-SW). Pia ataagiza kwa uangalifu mzee yeyote au mtumishi wa huduma ambaye anaweza kusaidia kukusanya ripoti. Hilo litahakikisha hesabu sahihi ya habari inayohitajiwa kutoka kwa Maandishi ya Mhubiri ya Kundi (S-21-SW). Fomu ya Ripoti ya Mchanganuo wa Kutaniko (S-10-SW) yapasa kujazwa kwa usahihi na unadhifu na ichunguzwe vizuri na halmashauri ya utumishi.
◼ Ugavi wa kutosha wa fomu za kutumia wakati wa mwaka wa utumishi wa 1997 unapelekwa kwa kila kutaniko. Fomu hizi hazipaswi kutumiwa vibaya. Zapaswa kutumiwa tu kwa kusudi lazo.
◼ Makutaniko yapaswa kuanza kuagiza 1997 Calendar of Jehovah’s Witnesses pamoja na ombi lao la fasihi la Septemba. Kalenda zitapatikana katika Kichina, Kiingereza na Kifaransa.
◼ Kuanzia Agosti 28, 1996, hadi Agosti 31, 1996, Sosaiti itakuwa ikihesabu fasihi zote zilizo katika tawi na depo mbalimbali. Kwa sababu ya kuhesabu huku, hakuna maagizo yoyote ya fasihi ya kutaniko yatakayofanyiwa upakizi au yatakayochukuliwa siku hizo.