Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 7/97 uku. 4
  • Saidia Wengine Wapate Faraja

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Saidia Wengine Wapate Faraja
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Habari Zinazolingana
  • Mwige Yehova kwa Kujali Wengine Kikweli
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Tangaza Habari Njema za Ufalme Ukitumia Broshua
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Tumia Broshua Mbalimbali Katika Huduma Yako
    Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Jinsi ya Kutumia Broshua Habari Njema Kutoka kwa Mungu!
    Huduma ya Ufalme—2013
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1997
km 7/97 uku. 4

Saidia Wengine Wapate Faraja

1 Watu wengi wamechoka kusikia juu ya misiba, vita, uhalifu, na kuteseka. Faraja, ingawa haipo katika ripoti za habari za leo, ni kitu ambacho kwa kweli mwanadamu anakihitaji. Kufariji humaanisha “kupatia nguvu na tumaini” na “kutuliza kihoro au taabu ya” mwingine. Tukiwa Mashahidi wa Yehova, tumeandaliwa vifaa ili kusaidia watu katika njia hii. (2 Kor. 1:3, 4) Broshua zetu zenye kutegemea Biblia ambazo tutakuwa tukitoa katika Julai na Agosti zina ujumbe wa kweli wenye kufariji. (Rom. 15:4) Hapa pana madokezo kadhaa ya kuzitoa chini ya hali mbalimbali:

2 Hadithi ya habari yenye kuhuzunisha yaweza kutokeza fursa ya kutoa ushahidi na kuletea wengine faraja, labda kwa kusema jambo kama hili:

◼ “Mambo kama hayo yatokeapo, watu wengine hujiuliza kama kweli Mungu yuko, na ikiwa yuko, kama anatujali. Wafikirije? [Ruhusu itikio.] Njia moja ya kuamua kama kuna Mungu ni kutumia vizuri kanuni iliyothibitishwa.” Soma Waebrania 3:4. Onyesha mambo mengine yanayotuzunguka ambayo kwa wazi yalihitaji mfanyi. Kisha endelea: “Nina broshua ambayo najua utaiona kuwa yenye kufariji. Ina kichwa Je! Kweli Mungu Anatujali? [Soma maswali yaliyo kwenye jalada.] Ina uthibitisho wenye kusadikisha kwamba Mungu yuko na pia kwamba hivi karibuni atakomesha hali zote zisizofaa tunazokabili leo. Je, ungependa kuisoma? Twaiacha kwa mchango mdogo wa ________ .” Panga urudi.

3 Katika ziara ya kurudia, unaweza kusema hivi:

◼ “Tulikuwa tukizungumza juu ya uthibitisho wa kuwapo kwa Mungu nilipokuachia ile broshua Je! Kweli Mungu Anatujali? Labda uliona hoja hii kwenye ukurasa wa 7. [Onyesha picha na uzungumzie kifupi fungu la 15.] Hiki ni kielelezo kimoja tu cha kuonyesha kwamba Mungu mwenye kujali lazima awepo. [Soma fungu la 27 kwenye ukurasa wa 9.] Funzo la Biblia la kibinafsi limenisaidia kukabiliana na matatizo ya maisha ya leo kwa sababu hutoa maoni ya Mungu kuhusu mambo.” Onyesha jinsi ya kujifunza.

4 Ushahidi wa simu mahali panapowezekana waweza kutumiwa ukitumia broshua “Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai?—Wewe Waweza Kulipataje?” Unaweza kujijulisha na kusema:

◼ “Nakupigia simu nikiwa na ujumbe wa maana kwa sababu siwezi kukuona kibinafsi.” Soma fungu la kwanza kwenye ukurasa wa 4 wa broshua hiyo, ukifanya hivyo kwa njia ya kawaida, kana kwamba unazungumza na mtu huyo kibinafsi. Mwulize analofikiria, na uruhusu itikio. “Nimefungua Biblia yangu kwenye Isaya 45:18. Mstari huu waonyesha dunia iliumbwa kwa ajili yetu. Je, nikusomee?” Baadaye, eleza sababu ya broshua hiyo, na uulize jinsi ambavyo ungeweza kumpelekea nakala moja.

5 Katika kufuatia tena kwa njia ya simu, unaweza kujaribu mfikio huu ili kuanzisha funzo:

◼ “Ningependa kuendeleza mazungumzo yetu ya wakati uliopita kwa kutoa kielezi cha kuonyesha ni nani awezaye kutuambia kusudi la uhai. [Simulia kwa maneno mengine fungu la 1 na la 2 kwenye ukurasa wa 6 katika broshua Kusudi la Uhai.] Ufunuo 4:11 hueleza kwamba Yehova Mungu ndiye Muumba wetu. [Soma.] Kwa hakika lazima alikuwa na sababu ya kutuumba. Watu ambao wametaka kuijua sababu hiyo wamejifunza Neno la Mungu lililoandikwa, Biblia. Ningependa kukutolea fursa hiyo.” Eleza jinsi mtaala wa funzo letu la Biblia nyumbani bila malipo unavyofanywa, kisha ufanye mipango ya kuanzisha funzo.

6 Mfikio huu unaofaa waweza kufariji wale ambao wamefiwa na mpendwa:

◼ “Natoa utumishi wa watu wote kwa niaba ya wale ambao wamepoteza mpendwa katika kifo. Kwa kuwa hili huenda likawa mojawapo ya mambo magumu kwa yeyote kati yetu kukabiliana nayo, broshua hii, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, imetayarishwa. Imesaidia mamilioni ya watu. Ningependa kukuonyesha inayosema juu ya ahadi yenye kusisimua iliyotolewa na Yesu Kristo. [Soma fungu la tano kwenye ukurasa wa 26, kutia ndani Yohana 5:21, 28, 29.] Angalia picha hii kwenye ukurasa wa 29 inayoonyesha kwa kweli simulizi la Gospeli kuhusu Yesu akimfufua Lazaro kutoka kwa wafu. Ikiwa ungependa kusoma broshua hii yenye kufariji, nitafurahi kukuachia kwa mchango mdogo wa ________ .”

7 Unaporudi, unaweza tena kuonyesha picha iliyo kwenye ukurasa wa 29 wa broshua “Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa” na useme:

◼ “Kumbuka mazungumzo yetu juu ya Kristo kumfufua Lazaro. [Soma maelezo ya picha kwenye ukurasa wa 28, na mzungumzie habari yenye kichwa kidogo “Je! Kweli Hilo Lilitukia?”] Moyo wako ukitamani sana kuamini kwamba unaweza kumwona tena mpendwa aliyekufa, acha nikusaidie uwe na tumaini la ufufuo.” Mtolee funzo la Biblia nyumbani.

8 Na tufanye yote tuwezayo miezi inayokuja tumwige Yesu kwa “kuwafariji wote waliao.”—Isa. 61:2.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki