Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 1/98 uku. 4
  • Ona Upendezo Katika Kutoa Ushahidi Kamili

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ona Upendezo Katika Kutoa Ushahidi Kamili
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Habari Zinazolingana
  • Hubiri kwa Ufahamu Wenye Kina
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Habari Unazoweza Kutumia Katika Utumishi wa Shambani
    Huduma ya Ufalme—2005
  • Kutumia Vizuri Vitabu Vyetu vya Zamani
    Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Ujuzi Kutoka kwa Mungu Hujibu Maswali Mengi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 1/98 uku. 4

Ona Upendezo Katika Kutoa Ushahidi Kamili

1 Sisi sote hufurahia kufanya mambo tuyafanyayo vema. Marko 7:37 husema kwamba umati ulitangaza hivi kumhusu Yesu: “Amefanya mambo yote vema.” Si ajabu kwamba Yesu aliona upendezi katika kufanya mapenzi ya Yehova! (Linganisha Zaburi 40:8.) Kwa kufikiria madokezo yafuatayo, sisi vilevile tutapata shangwe tunapotii amri ya Yesu ya “[k]uwahubiri watu na kutoa ushahidi kamili.” (Mdo. 10:42) Januari tunatoa kitabu chochote chenye kurasa 192 kilichochapishwa kabla ya 1985 ambacho huenda ikawa kutaniko linacho akibani au kitabu Usalama Ulimwenguni Pote Chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani.” Twaweza kutumiaje vichapo hivi kutoa ushahidi kamili?

2 Kwa kuwa mara nyingi watu wanahangaika juu ya masuala ya afya, unaweza kusema hivi:

◼ “Ujapokuwa utimizo mbalimbali uliofanywa upande wa kitiba, kuna kuteseka kwingi kwa sababu ya ugonjwa. Kwa maoni yako, kwa nini hali iko hivyo? [Ruhusu itikio.] Yesu Kristo alisema kwamba ugonjwa wa kuambukiza ungekuwa sehemu moja kuu ya siku za mwisho. (Luka 21:11) Na bado pia Biblia hufafanua wakati ambapo ugonjwa hautakuwapo tena. [Soma Isaya 33:24.] Ona jinsi ambavyo kitabu hiki hutokeza tumaini katika fundisho hilo la msingi la Biblia.” Kazia maelezo yafaayo katika kitabu ambacho unatoa, na ukitoe.

3 Unapotoa ushahidi wa vivi hivi karibu na maeneo ya duka, ungeweza kumsalimu kisha uulize:

◼ “Je, yaonekana kwako kwamba vitu vyaendelea kuwa ghali sana hata kwamba ni vigumu kuvilipia? [Ruhusu itikio.] Je, wafikiri kwa vyovyote wakati utafika ambapo kutakuwa na usalama wa kweli wa kiuchumi?” Ruhusu itikio. Kisha utoe nukuu la Andiko linalofaa kutoka katika kitabu unachotoa. Endelea kwa kusema: “Kitabu hiki chaonyesha jinsi ambavyo, kupitia Ufalme wake, Mungu atatatua matatizo yanayofanya maisha yawe magumu sana leo.” Toa kitabu kwa mchango uliopendekezwa. Unaweza kusema jinsi ambavyo umefurahia mazungumzo kisha uulize: “Je, kuna njia yoyote tuwezayo kuendelea na mazungumzo haya wakati mwingine?” Kwa njia hii huenda ukaweza kupata namba ya simu au anwani ya nyumbani ya huyo mtu.

4 Huenda ukawa na fursa ya kujaribu utoaji huu kuhusu amani ya ulimwenguni, ukitumia kitabu “Usalama Ulimwenguni Pote”:

◼ “Kwa maoni yako, kwa nini ni vigumu kupata amani ya ulimwenguni? [Ruhusu itikio, kisha soma Ufunuo 12:7-9, 12.] Ukosefu wa amani ya ulimwenguni ni mojawapo ya matokeo ya kutupwa kwa Ibilisi chini mpaka kwenye dunia. Kitabu hiki chaonyesha kwamba tamaa ya amani na usalama ulimwenguni pote itatimizwa na Ufalme wa Mungu. [Onyesha picha iliyoko kwenye ukurasa wa 3-4.] Soma kichwa cha sura ya 1 na utoe kitabu hicho.

5 Unaporudi kuona wale ambao wameonyesha kupendezwa, unaweza kujitahidi kuanzisha funzo la Biblia kwa kujipatanisha na mfikio huu:

◼ “Mara ya mwisho tulipoongea, ulitoa maoni yenye kupendeza sana. [Taja elezo ambalo mtu huyo alitoa.] Nimekuwa nikilifikiria, nami ningependa kushiriki matokeo ya utafiti niliofanya wa habari hiyo. [Shiriki andiko lifaalo.] Twajitolea kuongoza mtaala wa funzo bila malipo ambao umewezesha mamilioni ya watu wachunguze mafundisho ya msingi ya Biblia kwa kipindi kifupi cha wakati. Uchunguzi huo waweza kujenga uhakika wako katika utimizo wa ahadi za Mungu.” Kazia baadhi ya maswali ambayo yatajibiwa. Mtu huyo akikataa funzo la Biblia, mweleze kwamba pia tuna mtaala wa kuharakisha ambao huchukua dakika 15 tu kila juma kwa majuma 16. Onyesha broshua Anataka, fungua somo la 1, na uulize kama unaweza kumwonyesha jinsi ya kujifunza somo la kwanza.

6 Kumbuka Kutumia Vikaratasi vya Kukaribisha Watu: Vyaweza kutumiwa kwa matokeo katika utangulizi wako ili kuchochea kupendezwa katika mambo ya kiroho, au vyaweza kutolewa ikiwa fasihi haikukubaliwa. Mahali watu walipopendezwa, tumia ujumbe uliochapwa nyuma ya kikaratasi hicho kutia moyo mtu akubali funzo la Biblia nyumbani na aje kwenye mikutano yetu.

7 Uwe mwenye ustadi katika kazi yako, na utapata shangwe katika hiyo. Kazia uangalifu daima kutoa ushahidi kamili, na uone upendezo katika kuzifanya vema sehemu zote za huduma.—1 Tim. 4:16.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki