Habari Za Kitheokrasi
Kuwekwa Wakfu kwa Ofisi ya Tawi: Jumamosi, Oktoba 25, 1997, ndugu 1,697 kutoka nchi 26 walihudhuria programu ya pekee ya kuwekwa wakfu kwa ofisi ya tawi mpya Nairobi. Programu hiyo ilirudiwa Jumapili, Oktoba 26, 1997, kwenye Jamhuri Park, Nairobi na watu 10,145 walihudhuria. Ilikuwa shangwe kukutana na kushirikiana na watu wa zamani katika eneo letu na kutoka nchi nyinginezo. Kwa kweli kulikuwako na kitia-moyo kwa wote. Wale wanaotaka kuzuru Betheli mpya wanakaribishwa kufanya hivyo wakati wa saa za kazi za Betheli.
Jumba la Ufalme: Jumba la Ufalme la Mbeya Ruanda katika Tanzania liliwekwa wakfu hivi majuzi.