Matangazo
◼ Toleo la fasihi la Machi: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Kazia kuanzisha mafunzo ya Biblia nyumbani. Aprili na Mei: Maandikisho ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mahali ambapo maandikisho hayachukuliwi, toa magazeti yote mawili kwa mchango wa kawaida au broshua Mungu Anataka Tufanye Nini? Juni: Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi, Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu, au kitabu chochote chenye kurasa 192.
◼ Wahubiri wanaotaka kutumikia wakiwa mapainia-wasaidizi katika Aprili na Mei wapaswa kufanya mipango yao sasa na kuleta fomu yao ya ombi mapema. Kufanya hivyo kutasaidia wazee wafanye mipango ya lazima ya utumishi wa shambani na kuwa na magazeti ya kutosha na fasihi nyingine. Kutaniko lapaswa litangaze majina ya wote wanaokubaliwa kuwa mapainia-wasaidizi.
◼ Mapainia wa kawaida wanaopendezwa na kushiriki katika kampeni ya mwaka huu ya eneo lililo peke yake kuanzia Julai hadi Septemba wakiwa mapainia wa pekee wa muda, sasa wanaweza kutoa ombi kupitia halmashauri ya utumishi ya kutaniko lao. Halmashauri ya utumishi ya kutaniko yapaswa kuandaa habari ya ziada kuhusu mwenye kutoa ombi. Tungependa kujua kama mwenye kutoa ombi ni mseja au amefunga ndoa, ana watoto au hana. Barua ya kupendekeza yapaswa kufikia ofisi ya tawi Aprili 1, 1998 ikiwa itakawia.
◼ Mwangalizi-Msimamizi au mtu fulani aliyeteuliwa naye apaswa kukagua hesabu ya kutaniko Machi 1 au upesi iwezekanavyo baada ya hapo. Tangazieni kutaniko jambo hilo lifanywapo.
◼ Wale wanaoshirikiana na kutaniko wapaswa kupeleka maandikisho yote mapya na ya kufanywa upya ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni!, kutia ndani maandikisho yao ya kibinafsi, kupitia kutaniko.
◼ Sosaiti haishughulikii maagizo ya fasihi ya wahubiri mmoja-mmoja. Mwangalizi-Msimamizi apaswa kupanga tangazo lifanywe kila mwezi kabla ya agizo la kila mwezi la fasihi la kutaniko halijapelekwa kwa Sosaiti ili wote wenye kupendezwa kupata fasihi ya kibinafsi waweze kumjulisha ndugu anayeshughulikia fasihi. Tafadhali kumbuka ni vichapo gani vilivyo vifaa vya kuagizwa kipekee.
◼ Vichapo Vipya Vinavyopatikana:
Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote—Kifaransa, Kiingereza, Kiswahili
Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu—Kiswahili