Kikumbusha
Katika eneo letu tuna Majumba kadhaa ya Ufalme yanayotumiwa lakini hayajawekwa wakfu bado. Majumba ya Ufalme fulani hayajakamilika bado ijapokuwa yanatumiwa. Twatia moyo mabaraza ya wazee na Halmashauri za Ujenzi za Kimkoa wahakikishe linaloweza kufanywa ili Majumba ya Ufalme hayo ambayo hayajakamilishwa, baadhi yake yakiwa na kazi chache zilizobaki, yamalizwe na kuwekwa wakfu. Kitabu Tumefanywa Tengenezo Tutimize Huduma Yetu kwenye ukurasa wa 61 husema kwamba inafaa kuwa na programu ya kuweka wakfu. Ingawa kusudi la Jumba la Ufalme ni kutumiwa, limepasa liwe mahali pa kustarehesha na penye kufaa kuongozea mikutano ya Kikristo inayotusaidia tukue kiroho na kujifunza juu ya Yehova, na inayotutia moyo tushiriki utumishi wake wa Ufalme. (Ebr. 10:23-25; Mt. 24:14; 28:19, 20) Je, Jumba la Ufalme lenu halijakamilishwa? Ni nini kinachohitaji kufanywa ili kulimaliza na kuliweka wakfu?