Matangazo
◼ Toleo la fasihi la Februari: Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Mahali ambapo hakipatikani, toa kitabu Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha. Machi: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Jitihada ya pekee itafanywa kuanzisha mafunzo ya Biblia ya nyumbani. Aprili na Mei: Maandikisho ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mahali ambapo andikisho halichukuliwi, toa magazeti yote mawili kwa mchango wa kawaida. Uwe na broshua Anataka kwa ajili ya watu wenye kupendezwa, na ujitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia.
◼ Mapainia wa kawaida wanaopendezwa kushiriki katika kampeni ya mwaka huu ya eneo lililo pekee kuanzia Julai hadi Septemba wakiwa mapainia wa pekee wa muda hawatahitaji kutoa ombi kwa Sosaiti. Hata hivyo, wanaweza kumjulisha mwangalizi wa mzunguko kwamba wanapendezwa kutumikia wakiwa mapainia wa pekee wa muda.
◼ Kuanzia juma la Machi 22, 1999, kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi kitachunguzwa katika Funzo la Kitabu la Kutaniko. Toleo hili la Huduma ya Ufalme Yetu lina ratiba kamili ya funzo. Unaweza kufanya fotokopi na kuiweka katika nakala yako ya kibinafsi ya kitabu ili ipatikane kwa ajili ya marejezo au unaweza kuweka toleo hili la Huduma ya Ufalme Yetu mahali liwezapo kupatikana kwa urahisi kwa ajili ya marejezo. Mwelekezo wa jinsi utangulizi wa kitabu utakavyofanywa waelezwa katika fungu la tano la “Kujifunza Kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi” kwenye ukurasa wa 3 wa Huduma ya Ufalme Yetu ya Julai 1993.
◼ Mwandishi na mwangalizi wa utumishi wanapaswa kupitia utendaji wa mapainia wote wa kawaida. Ikiwa kuna wowote wanaopata ugumu wa kutimiza takwa la saa, wazee wapaswa kupanga ili usaidizi utolewe. Ili kupata madokezo, pitia barua za kila mwaka za Sosaiti (S-201-SW) za Oktoba 1. Ona pia fungu la 12-20 la nyongeza ya Huduma ya Ufalme Yetu ya Septemba 1986.