Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 3/01 uku. 7
  • Matangazo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Matangazo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2001
Huduma Yetu ya Ufalme—2001
km 3/01 uku. 7

Matangazo

◼ Toleo la Machi: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele na Wenye Umoja Katika Ibada ya Mungu wa Pekee wa Kweli. Jitihada ya pekee itafanywa ili kuanzisha mafunzo ya Biblia ya nyumbani. Aprili na Mei: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Unapopata watu wenye kupendezwa kwenye ziara za kurudia, waweza kutoa maandikisho. Toa kitabu Ujuzi au broshua Anataka, ukiwa na lengo la kuanzisha mafunzo ya Biblia ya nyumbani. Juni: Mungu Anataka Tufanye Nini? au Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Jitahidini kuanzisha mafunzo ya Biblia ya nyumbani.

◼ Wahubiri wanaotaka kutumikia wakiwa mapainia-wasaidizi mwezi wa Aprili wanapaswa kuanza kufanya mipango sasa na kujaza na kupeleka fomu ya ombi lao mapema. Hilo litasaidia wazee wafanye mipango ifaayo ya utumishi wa shambani na kupanga kuwe na magazeti ya kutosha na vichapo vinginevyo. Majina ya wale wanaokubaliwa kuwa mapainia-wasaidizi yapasa kutangazwa kutanikoni.

◼ Ukumbusho utafanywa Jumapili, Aprili 8, 2001. Hakuna mikutano mingine itakayofanywa siku hiyo isipokuwa ile ya utumishi wa shambani. Wazee wanaweza kufanya mipango inayofaa ili Funzo la Mnara wa Mlinzi lifanywe wakati mwingine.

◼ Wale wanaoshirikiana na kutaniko wapaswa kutuma maandikisho yote mapya na yaliyoandikishwa upya ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni!, kutia ndani maandikisho ya kibinafsi, kupitia kutaniko.

◼ Sosaiti haikubali maagizo ya vichapo ya wahubiri mmoja-mmoja. Mwangalizi-msimamizi apaswa kupanga tangazo lifanywe kila mwezi kabla ya agizo la kila mwezi la vichapo la kutaniko halijapelekewa Sosaiti, ili wote ambao wanataka kupata vichapo vya kibinafsi waweze kumjulisha ndugu anayeshughulikia vichapo. Tafadhali kumbuka ni vichapo gani ambavyo vinapasa kuagizwa kipekee.

◼ Itafaa vikundi vya watu 20 au zaidi wakipanga kutembelea ofisi ya tawi ya Sosaiti wawasiliane na ofisi mapema kupitia barua. Kabla ya kutembea, tafadhali pitieni Sanduku la Swali la Huduma Yetu ya Ufalme ya Machi 1998 kuhusu mavazi na mapambo yanayofaa mnapotembelea makao ya Betheli.

◼ Habari ya kisheria yapatikana ya kusaidia wahubiri ambao wanahusika katika kesi za mahakamani za malezi ya watoto na haki ya kutembelea watoto zinazohusu dini yetu. Habari hiyo yapasa kuombwa na baraza la wazee katika kisa tu ambapo ni dhahiri kwamba itikadi za kidini za mhubiri zitahusika. Kwa wale wanaokabiliwa na masuala ya kawaida juu ya malezi ya mtoto au haki ya kutembelea watoto, habari yenye msaada yaweza kupatikana katika gazeti la Amkeni! la Desemba 8, 1997, ukurasa wa 3-12; katika Amkeni! la Oktoba 22, 1988, ukurasa wa 2-14 (toleo la Kiingereza); na kwenye chati inayopatikana katika Amkeni! la Oktoba 8, 1991, ukurasa wa 9.

◼ Kikumbusha: Haifai kuacha simu za mkononi bila kuzimwa unapokuwa kwenye mikutano ya kutaniko na makusanyiko. Hatutaki kukengeusha fikira za wasikilizaji kwa njia yoyote ile wanaposikiliza programu ya kiroho iliyotayarishwa kwa wakati huo.

◼ Vichapo Vipya Vinavyopatikana:

Vichwa vya Mazungumzo vya Biblia—Kiamhara

Sikiliza Unabii wa Danieli!—Kitigrinya

Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli?—Kiganda, Kizande

Mungu Anataka Tufanye Nini?—Kichina Sahili (Kipinyin)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki