Tenga Wakati wa Kutoa Magazeti
1 Yehova ameamua kwamba kutakuwako ‘amani, wakati ujao, na tumaini’ kwa wale wanaofuata njia zake. (Yer. 29:11) Habari inayohusu taraja hili yapatikana kwa wakati unaofaa katika Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Magazeti haya yanaweza kunufaisha watu wa aina zote wenye hali mbalimbali. (1 Tim. 2:4) Je, wewe na familia yako hutenga wakati wa kugawanya magazeti kwa ukawaida?
2 Ikiwa utoaji wako wa magazeti umepungua, jambo hilo laweza kurekebishwaje? Jambo moja muhimu ni kuendelea kuthamini habari iliyomo ndani ya magazeti yetu. Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! ni vifaa vilivyofanyiwa utafiti kwa uangalifu na ni maandalizi ya “mtumwa mwaminifu na mwenye busara.” (Mt. 24:45) Magazeti hayo ni vifaa vyenye matokeo vinavyofikia mioyo ya watu.
3 Yasome magazeti unayotoa. Tafuta habari zinazoshughulika na matatizo yanayoikumba jamii yako sasa. Jitayarishe kuonyesha jinsi magazeti yanavyofaa watu mmoja-mmoja na familia kwa ujumla.