Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 11/01 uku. 5
  • Jihadhari na Misemo ya Kawaida ya Ushirikina

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jihadhari na Misemo ya Kawaida ya Ushirikina
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2001
Huduma Yetu ya Ufalme—2001
km 11/01 uku. 5

Jihadhari na Misemo ya Kawaida ya Ushirikina

Watu wengi hutumia misemo kama hii: “Tuna bahati kupata mtoto”; “Kwa bahati mbaya sikufuzu mtihani”; “Alipatwa na ajali ya ndege au ya gari.”

Misemo hiyo ina ubaya gani? Ni nini maana ya “bahati” na “ajali”? Biblia hujibu hivi kwenye Isaya 65:11, kulingana na New World Translation of the Holy Scriptures: “Lakini nyinyi watu ndio wale wanaomwacha Yehova, wale wanaousahau mlima wangu mtakatifu, wale wanaoandaa meza kwa ajili ya mungu wa Bahati Nzuri [“yule roho mwovu”; Kilatini, Fortunae, kielezi-chini katika NW] na wale wanaojaza divai iliyochanganywa kwa ajili ya mungu wa Ajali.” Wakati Wayahudi waasi-imani katika siku za Isaya walipoanza kutegemea ‘mungu wa Bahati Nzuri na mungu wa Ajali,’ walikuwa wakimwacha Yehova. Japo walikuwa bado wakitoa ibada fulani kwenye hekalu lake, ilikuwa desturi tu, kwani waliheshimu ‘mungu wa Bahati Nzuri na mungu wa Ajali’ mioyoni mwao. Kwa sababu hiyo, Yehova alisema hivi: “Nitawaandikia kuuawa kwa upanga, na ninyi nyote mtainama ili kuchinjwa.” (Isa. 65:12) Hivyo, watu wanapotumia misemo ya kawaida ya ushirikina iliyotajwa juu, wao huheshimu ‘mungu wa Bahati Nzuri na mungu wa Ajali’ pasipo kujua. Bila shaka, hungependa kuwa kati yao na kufanya wengine wafikiri kwamba wewe ni mwabudu wa “Bahati Nzuri.” Badala yake, unataka watu wajue kwamba huna uhusiano wowote na misemo hiyo ya ushirikina. Naam, ukitumia misemo hiyo, huenda wengine wakafikiri wewe pia unaamini kwamba hali nzuri au mbaya huletwa na bahati. Utimizo wa maneno ya Isaya ulitokeza msiba wa taifa lote wakati Yehova alipoacha taifa hilo lishambuliwe na Babiloni ya kale yenye uweza mwaka wa 607 K.W.K. Miungu ya Wayahudi ya “Bahati Nzuri” na “Ajali” haikuzuia jiji la Yerusalemu lisiharibiwe kabisa. Kwa hiyo, mtu anapoamini ushirikina, yeye huacha kumwamini na kumtegemea Mungu Mweza Yote. (it-1 973; g81-E 6/8 4; g92-E 6/8 11; g65-E 27-28; gh-E 133-140) Ili upate habari zaidi kuhusu Bahati na Ajali, tafadhali ona matoleo ya Aprili na Agosti 1976 ya Utumishi Wetu wa Ufalme, chini ya kichwa “BAHATI NA AJALI.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki