Matangazo
◼ Toleo la vichapo la Juni: Mungu Anataka Tufanye Nini?, Wewe Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu!, au kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Ikiwa wenye nyumba tayari wana vichapo hivyo, kitabu Wenye Umoja Katika Ibada ya Mungu wa Pekee wa Kweli chaweza kutolewa. Julai na Agosti: Broshua yoyote kati ya broshua zifuatazo zenye kurasa 32 yaweza kutumiwa: Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je! Uamini Utatu?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Ni Nini Hutupata Tunapokufa?, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?, Serikali Itakayoleta Paradiso, na “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya.” Broshua Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?, Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli?, na Our Problems—Who Will Help Us Solve Them? zaweza kutolewa inapofaa. Vijitabu Je! Kuna Mungu Anayejali?, Roho Zisizoonekana—Je! Zinatusaidia? Au Zinatuumiza? na God’s Way Is Love zaweza kutolewa pia. Septemba: Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation? au Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
◼ Tarehe za makusanyiko ya wilaya yafuatayo ya Tanzania zimebadilishwa: Sumbawanga na Songea zitakuwa Agosti 2-4, 2002, badala ya Agosti 3, 4, 2002. Bukoba itakuwa Agosti 23-25, 2002, badala ya Agosti 24, 25.
◼ Darasa la 11 la Shule ya Mazoezi ya Kihuduma nchini Kenya lilihitimu Novemba 4, 2001. Shule hiyo yaendelea kuandaa mazoezi yanayofaa kwa akina ndugu ambao wako tayari kujitolea kushiriki zaidi katika kazi ya mavuno. (Mt. 9:36, 37) Wazee na watumishi wa huduma ambao ni waseja, wenye umri wa kati ya miaka 23-50, wanaojua Kiingereza au Kifaransa na wanapendezwa na shule hiyo, wanaweza kuhudhuria mkutano wa wale ambao wangependa kuhudhuria shule hiyo kwenye kusanyiko la mzunguko litakalofuata.
◼ Fomu za kila mwaka za kutaniko zitatumwa zikipatikana. Maagizo kuhusu jinsi ya kuzigawanya fomu hizo yatapatikana kwenye orodha ya upakizi. Ikiwa makutaniko zaidi ya moja yanatumia Jumba la Ufalme, mratibu wa vichapo anapaswa kuhakikisha kwamba kila kutaniko linapokea fomu zake mara tu zifikapo.
◼ Mwangalizi-msimamizi au mtu fulani aliyeteuliwa naye apaswa kukagua hesabu ya kutaniko Juni 1 au upesi iwezekanavyo baada ya tarehe hiyo. Jambo hilo lifanywapo, tangazieni kutaniko baada ya ripoti ya hesabu kusomwa.
◼ Gazeti la Amkeni! la Kiurdu litaacha kuchapishwa mara moja kwa mwezi liwe likichapishwa baada ya kila miezi mitatu, kuanzia toleo la Aprili-Juni 2002.
◼ Vichapo Vipya Vinavyopatikana:
Je, Una Roho Isiyoweza Kufa? (Trakti Na. 25) —Kikamba, Kikuyu
◼ Video Mpya Zinazopatikana:
The Greatest Man Who Ever Lived—On Videocassette, Sehemu ya 8 —Lugha ya Ishara ya Marekani