Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 7/02 uku. 1
  • Jinsi Michango Yetu Inavyotumiwa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi Michango Yetu Inavyotumiwa
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 7/02 uku. 1

Jinsi Michango Yetu Inavyotumiwa

1 Kazi ya ulimwenguni pote ya kufundisha Biblia ambayo Mashahidi wa Yehova hufanya, inagharimiwa kwa michango ya hiari. Fedha zote zinazopokewa hutumiwa kulipia gharama kubwa sana za kushughulikia kazi ya kuhubiri Ufalme nyakati hizi za kisasa. Mbali na kuchapisha vichapo vya kugawanywa ulimwenguni pote, Sosaiti hutunza ofisi za tawi, makao ya Betheli, shule za kihuduma na za mishonari, mishonari wenyewe, mapainia wa pekee, waangalizi wasafirio, vituo vya kugawanya vichapo, na huduma nyinginezo mbalimbali zinazohitajiwa ili kutimiza kazi ambayo Yesu aliwapa wanafunzi wake.—Mt. 24:14; 28:19, 20.

2 Wahubiri wengi na familia zao huzoea kuweka kando kiasi fulani ili kuchangia kazi ya ulimwenguni pote. (Linganisha 1 Wakorintho 16:1, 2.) Kwa njia hiyo, shughuli zote za Sosaiti zagharimiwa, kutia ndani kugawanywa kwa vichapo. Twendeleapo kupanua huduma yetu kwa bidii, tukitumia vichapo vyenye thamani vya Sosaiti kwa hekima, Yehova ataendelea kutupatia ongezeko. Watu wakarimu kila mahali wanathamini maelezo yetu yanayofaa kuhusu huduma yetu na wanafurahia kuunga mkono kazi yetu kwa kutoa michango yao ya hiari.

3 Sosaiti inawezaje kuwapatia watu wote vichapo bila malipo? Gharama zisizoepukika zinazotumiwa kuchapisha na kugawa vichapo hulipwa kwa michango ya hiari. Watumishi wa Yehova waliojiweka wakfu ndio wa kwanza kutoa michango hiyo. Mashahidi wa Yehova hawategemei watu wengine wagharimie kazi hii ya haraka sana ya kutangaza Ufalme. Hatujawahi kamwe kufanya harambee, wala hatufanyi harambee sasa. Hata hivyo, michango midogo kutoka kwa watu wenye kupendezwa na kutoka kwa wale wanaothamini tunaokuta shambani yathaminiwa.

4 Kwa kumalizia, akina ndugu katika eneo letu kama wale wengine ulimwenguni hukumbuka kwamba watu wa Yehova waliojiweka wakfu ndio wa kwanza kutoa fedha zinazohitajiwa ili kuendeleza kazi ya ulimwenguni pote. Wanajua uhitaji huo nao huweka kwa ukawaida michango yao kwenye masanduku ya michango yaliyo katika Majumba yao ya Ufalme ambayo yameandikwa “Michango kwa Ajili ya Kazi ya Ulimwenguni Pote.—Mathayo 24:14.” Hilo lafanywa kwa hiari na kwa furaha kulingana na uwezo wa kila mtu kupatana na kanuni iliyo kwenye 2 Wakorintho 9:7. Wakati ripoti ya hesabu inaposomwa mbele ya kutaniko kila mwezi akina ndugu wanajulishwa kiasi kilichotumwa kwa Sosaiti kwa ajili ya kazi ya ulimwenguni pote na hivyo wanatiwa moyo kwa kujua kwamba kutaniko lao linachangia kazi ya Ufalme kwa ukawaida. Uwe na uhakika kwamba michango yako ya ukarimu kwa kazi ya Sosaiti ya ulimwenguni pote husaidia kutimiza kazi ya kuhubiri Ufalme na kufanya wanafunzi kotekote ulimwenguni.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki