Matangazo
◼ Toleo la vichapo la Septemba: Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!, Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani, au Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation? Oktoba: Gazeti la Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Watolee watu wanaopendezwa broshua Anataka, na ujitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia. Novemba: Mungu Anataka Tufanye Nini? au Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Iwapo watu tayari wana vichapo hivyo, kitabu kimoja cha zamani kitaweza kutolewa. Desemba: Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Vitabu vifuatavyo vinaweza kutumiwa pia: Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?, Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia, au Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani.
◼ Huduma Yetu ya Ufalme ya Oktoba 2002 inapaswa kugawanywa baada ya kutaniko kuhudhuria kusanyiko la wilaya.
◼ Wazee wanakumbushwa watekeleze maagizo yaliyotolewa kwenye ukurasa wa 21-23 wa toleo la Mnara wa Mlinzi, la Aprili 15, 1991, kuhusu kuwatembelea watu wowote waliotengwa na ushirika au waliojitenga, ambao huenda wakaonyesha mwelekeo wa kutaka kurudishwa.
◼ Ofisi ya tawi haishughulikii maagizo ya vichapo ya mhubiri mmoja-mmoja. Mwangalizi msimamizi anapaswa kupanga ili tangazo litolewe kila mwezi kabla ya agizo la kutaniko kutumwa kwenye ofisi ya tawi ili wote ambao wanataka kuagiza kichapo fulani waweze kumjulisha ndugu anayeshughulikia vichapo. Tafadhali shughulikieni ifaavyo bidhaa za kuagizwa kipekee.
◼ Gazeti la Mnara wa Mlinzi litapatikana kwenye video katika Lugha ya Ishara ya Marekani mara moja kwa mwezi kuanzia toleo la Septemba 1, 2002.
◼ Nyakati nyingine makutaniko na mhubiri mmoja-mmoja hukabili matatizo ya kisheria kuhusiana na ibada ya Yehova. Kijitabu Defending and Legally Establishing the Good News kilichochapishwa mwaka wa 1950 kilitoa maagizo kuhusu mambo hayo. Ijapokuwa kijitabu hicho kilikuwa na manufaa hapo awali, habari zake za kisheria hazifai wakati huu. Kwa hiyo, mabaraza ya wazee au wahubiri hawapaswi kutumia habari zilizomo katika kijitabu hicho ili kujaribu kusuluhisha matatizo ya kisheria.
◼ Hotuba ya pekee ya majira ya Ukumbusho mwaka wa 2003 itatolewa Jumapili, Aprili 27. Kichwa cha hotuba na muhtasari wa hotuba hiyo zitatangazwa baadaye. Makutaniko yatakayokuwa na ziara ya mwangalizi wa mzunguko au kusanyiko mwishoni mwa juma hilo, yatapanga hotuba ya pekee itolewe juma linalofuata. Hotuba ya pekee haipaswi kutolewa kabla ya Aprili 27, 2003 katika kutaniko lolote lile.
◼ Vichapo Vipya Vinavyopatikana:
Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi —Kiarabu, Kiswahili
Jinsi ya Kupata Maisha Yenye Kuridhisha—Kihindi
Unabii wa Isaya—Nuru kwa Wanadamu Wote II—Chapa Kubwa —Kiswahili
Does Fate Rule Our Lives?—Or Does God Hold Us Responsible? (kwa Waislamu) (Trakti Na. 71) —Kiurdu