Matangazo
◼ Toleo la vichapo la Novemba: Mungu Anataka Tufanye Nini? au Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Iwapo watu tayari wana vichapo hivyo, broshua Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele? au kitabu Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli au kitabu cha zamani chaweza kutolewa. Desemba: Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Kitabu hicho kisipopatikana, vitabu vifuatavyo vinaweza kutumiwa: Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?, Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia, au Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. Januari: Kitabu chochote kilichochapishwa kabla ya mwaka wa 1988 ambacho huenda kutaniko likawa nacho akibani. Pia Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo itatolewa. Ikiwa kutaniko halina toleo lolote kati ya hayo, tafadhali ulizeni makutaniko yoyote ya karibu kama yana vichapo vyovyote vya zamani vya ziada ambavyo mnaweza kutumia. Makutaniko ambayo hayana vitabu vya zamani yanaweza kutoa kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu. Februari: Mkaribie Yehova. Ikiwa hamna kitabu hicho mnaweza kutoa Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu! au Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation?
◼ Mwangalizi-Msimamizi au mtu fulani aliyeteuliwa naye apaswa kukagua hesabu ya kutaniko Desemba 1 au upesi iwezekanavyo baada ya tarehe hiyo. Jambo hilo lifanywapo, tangazieni kutaniko baada ya ripoti ya hesabu kusomwa.
◼ Makutaniko yanapaswa kuanza kuagiza mabuku yaliyojalidiwa ya Watchtower na Awake! ya mwaka wa 2003 pamoja na ombi lifuatalo la vichapo. Orodha ya lugha ambazo mabuku hayo yatapatikana itaonyeshwa katika “Tangazo kwa Makutaniko Yote,” ambalo hutumwa kwenye makutaniko yote kila mwezi. Hadi mabuku yaliyojalidiwa yapatikane na upakizi ufanywe, hayo yataonyeshwa chini ya “Vitatumwa Vikipatikana” katika orodha ya upakizi ya kutaniko. Mabuku yaliyojalidiwa ni bidhaa za ombi la pekee.
◼ Mwandishi wa kila kutaniko anapaswa kuhakikisha kwamba hati zote za umiliki za Jumba la Ufalme ziko sawa. Iwapo kuna barua zinazoonyesha kwamba kuna msamaha wa kutolipa ushuru au kodi hakikisheni kwamba ziko kwenye faili.
◼ Hundi za michango ambazo zimewekwa kwenye masanduku ya michango ya Jumba la Ufalme kwa ajili ya kazi ya ulimwenguni pote na Hazina ya Majumba ya Ufalme zinapaswa kuongezwa kwenye S-20 na kutumwa kwenye ofisi ya tawi.