Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/03 uku. 5
  • Pitio La Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Pitio La Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2003
Huduma Yetu ya Ufalme—2003
km 12/03 uku. 5

Pitio La Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi

Maswali yafuatayo yatashughulikiwa kwa njia ya maswali na majibu katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanzia Desemba 29, 2003. Mwangalizi wa shule atashughulikia pitio la dakika 30 linalotegemea habari iliyozungumziwa kwenye hotuba zilizotolewa juma la kuanzia Novemba 3 hadi Desemba 29, 2003. [Taarifa: Mahali ambapo vitabu vya marejezo havijatajwa baada ya swali, utahitaji kufanya utafiti wako mwenyewe ili kupata majibu.—Ona Shule ya Huduma, uku. 36-37.]

SIFA ZA USEMI

1. Kwa nini ni muhimu sana kutumia Biblia katika huduma ya shambani? [be uku. 145 fu. 2, sanduku]

2. Muktadha waweza kuathirije namna andiko linavyotangulizwa? [be uku. 149]

3. Kwa nini ni muhimu kukazia maneno yanayofaa unaposoma Biblia, na waweza kufanikiwaje kufanya hivyo? [be uku. 151 fu. 2, sanduku]

4. Tunawezaje kutumia shauri la Paulo la ‘kulitumia sawasawa neno la kweli’ tunapowafundisha wengine, na kwa nini jambo hilo ni muhimu? (2 Tim. 2:15) [be uku. 153 fu. 2, sanduku]

5. Paulo ‘alijadili namna gani kwa kutumia Maandiko’? (Mdo. 17:2, 3) [be uku. 155 fu. 5–uku. 156 fu. 1]

HOTUBA NA. 1

6. Tunapotumia Biblia ikiwa kitabu chetu kikuu cha utafiti kutayarisha hotuba, kwa nini ni muhimu (1) kuchunguza muktadha wa mistari, (2) kuchunguza marejeo, na (3) kutumia itifaki ya Biblia? [be uku. 34 fu. 3–uku. 35 fu. 2]

7. Uaminifu-mshikamanifu wa kweli unaonyeshwaje na kuelekea nani? [w01 10/1 uku. 22-23]

8. Ni jambo gani linaloonyesha kwamba Yehova hutunza wakati kwa usahihi? (Dan. 11:35-40; Luka 21:24) [si uku. 284 fu. 1]

9. Ni mambo gani unayopaswa kufikiria unapoamua ni mambo yapi utakayotumia katika hotuba baada ya kufanya utafiti? [be uku. 38]

10. Kwa nini maneno ambayo Yesu alisema kuhusu “siku za Noa” ni muhimu kwetu leo? (Mat. 24:37) [w01 11/15 uku. 31 fu. 3-4]

USOMAJI WA BIBLIA WA KILA JUMA

11. Barua ya Paulo kwa Filemoni yaonyeshaje kwamba utume wa Mkristo ni kusaidia watu wawe Wakristo wala si kuleta mabadiliko katika jamii? (Fil. 12)

12. Kuna tofauti gani kati ya ‘kupeperushwa mbali,’ “kujiondoa,” na ‘kuanguka’? (Ebr. 2:1; 3:12; 6:6) [w99 7/15 uku. 19 fu. 12; w86 6/1 uku. 14 fu. 16-17; w81 5/1 uku. 19 fu. 8 au w80-E 12/1 uku. 23 fu. 8]

13. Tunawezaje kuepuka kufanya msemo “ikiwa ni mapenzi ya Yehova” kuwa jambo lisilo na uzito? (Yak. 4:15) [cj-E uku. 171 fu. 1-2]

14. Yamaanisha nini ‘kungojea na kuweka karibu akilini kuwapo kwa siku ya Yehova,’ na twawezaje kufanya hivyo? (2 Pet. 3:12) [w97 9/1 uku. 19-20]

15. Ni shauri gani muhimu kwa Wakristo leo linalopatikana katika ujumbe kwa yale makutaniko saba yanayotajwa katika Ufunuo sura ya 2 na 3? (Ufu. 2:4, 5, 10, 14, 20; 3:3, 10, 11, 17, 19)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki