Matangazo
◼ Toleo la vichapo la Desemba: Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Kitabu hicho kisipopatikana, vitabu vifuatavyo vinaweza kutumiwa, Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?, Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia, au Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. Januari: Kitabu chochote kilichochapishwa kabla ya mwaka wa 1988 ambacho huenda kutaniko likawa nacho na pia Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Ikiwa kutaniko halina toleo lolote kati ya hayo, ulizeni makutaniko yoyote ya karibu kama yana vichapo vyovyote vya zamani vya ziada ambavyo mnaweza kutumia. Makutaniko ambayo hayana vitabu vya zamani yanaweza kutoa kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu. Februari: Mkaribie Yehova. Ikiwa hamna kitabu hicho, mnaweza kutoa kitabu Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu! au Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation? na Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Machi: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele na Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Jitihada za pekee zitafanywa ili kuanzisha mafunzo ya Biblia. Ikiwa watu tayari wana kichapo hicho, kitabu Sikiliza Unabii wa Danieli! kinaweza kutolewa.
◼ Ndugu wanaoshughulikia hesabu ya kutaniko wanapaswa kukumbuka kwamba michango iliyo kwenye masanduku ya Kazi ya Ulimwenguni Pote na Hazina ya Majumba ya Ufalme inapaswa kupelekwa kila mwezi na haipaswi kutumiwa kulipia mkopo wa Jumba la Ufalme au gharama nyingine za kutaniko.
◼ Mialiko ya Ukumbusho ya 2004 katika lugha kuu ya kila kutaniko itatumwa hivi karibuni. Ikiwa kuna lugha nyingine katika eneo lenu na mngependa mialiko ya lugha hizo, agizeni mialiko hiyo mara moja mkitumia Fomu ya Kuomba Vitabu (S-14). Orodha ya Mialiko ya Ukumbusho katika lugha mbalimbali itawekwa kwenye “Tangazo kwa Makutaniko Yote,” ambalo hutumwa kwa makutaniko yote kila mwezi. Tafadhali ombeni tu lugha zile zinazohitajiwa katika eneo lenu.
◼ Tungependa kuwajulisha kwamba Ukumbusho wa mwaka wa 2005 utakuwa Alhamisi, Machi 24, baada ya jua kutua. Taarifa hii imetolewa mapema ili akina ndugu waweze kufanya mapatano ya kukodi majumba mengine mahali ambapo makutaniko kadhaa yanatumia Jumba moja la Ufalme. Wazee wanapaswa kufanya maagano pamoja na wasimamizi wa jengo hilo ili kuhakikisha kwamba mwadhimisho wa Ukumbusho utaendelea kwa njia ya amani na kwa utaratibu bila kuvurugwa na utendaji mwingine katika jengo hilo. Kwa sababu ya umuhimu wa tukio hili, baraza la wazee linapaswa kumteua mzee mwenye kustahili zaidi atoe hotuba ya Ukumbusho badala ya kupokezana zamu tu au kutumia ndugu yuleyule kila mwaka. Ikiwa kuna mzee mwenye uwezo ambaye ni mtiwa-mafuta, apewe mgawo huo.
◼ Kuanzia juma la Machi 15, 2004, hadi Mei 16, 2005, tutajifunza kitabu Mkaribie Yehova katika Funzo la Kitabu la Kutaniko. Makutaniko yanayohitaji chapa kubwa ya kitabu hiki yanapaswa kuagiza kitabu hicho haraka iwezekanavyo.
◼ Makutaniko yanaweza kuagiza Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo itakayokuwa toleo la Januari, Februari, na Machi.
◼ Vitabu na magazeti yote yaliyopo yahesabiwe Desemba 31, 2003 au haraka iwezekanavyo baada ya tarehe hiyo. Hesabu hiyo ni kama ile inayofanywa kila mwezi na mratibu wa vitabu, na jumla ziandikwe kwenye fomu ya Orodha ya Vitabu (S-18). Jumla ya idadi ya magazeti yaliyopo inaweza kupatikana kutoka kwa watumishi wa magazeti. Mwandishi wa kutaniko linaloratibu anapaswa kusimamia kazi hiyo. Mwandishi na mwangalizi-msimamizi wa kutaniko linaloratibu watie sahihi fomu hiyo. Kila kutaniko linaloratibu litapokea nakala tatu za fomu ya Orodha ya Vitabu (S-18). Tafadhali tumeni nakala ya kwanza kwa ofisi ya tawi kabla ya Januari 6. Wekeni nakala ya kaboni kwenye faili zenu. Nakala ya tatu inaweza kutumiwa ili kufanyia hesabu.