Matangazo
◼ Toleo la vichapo la Mei: Toa magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Unapowarudia watu wanaopendezwa, kutia ndani wale ambao huhudhuria Ukumbusho au matukio mengine ya kitheokrasi lakini hawashirikiani na tengenezo, jitahidi kuwatolea kitabu Mwabudu Mungu. Jitahidi sana kuanzisha funzo la Biblia la nyumbani, hasa na watu ambao tayari wamejifunza kitabu Ujuzi na broshua Anataka. Juni: Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu. Watu fulani wakisema kwamba hawana watoto, watolee broshua Anataka. Jitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia ukitumia broshua hiyo. Julai na Agosti: Broshua yoyote kati ya broshua zifuatazo zenye kurasa 32 yaweza kutumiwa: Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je! Uamini Utatu?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Ni Nini Hutupata Tunapokufa?, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?, Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli?, Serikali Itakayoleta Paradiso, na “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya.”
◼ Mwangalizi-msimamizi au mtu fulani aliyeteuliwa naye apaswa kukagua hesabu ya kutaniko Juni 1 au upesi iwezekanavyo baada ya tarehe hiyo. Jambo hilo lifanywapo, tangazieni kutaniko baada ya ripoti ya hesabu kusomwa.
◼ Wanafunzi wa darasa la 15 la Shule ya Mazoezi ya Kihuduma nchini Kenya walihitimu Januari 25, 2004. Wanafunzi hao 24 walitoka Ethiopia, Kenya, Sudan, Tanzania, na Uganda. Programu hiyo iliwatia moyo sana wanafunzi na pia wale waliohudhuria. Ndugu waseja wenye umri wa kati ya miaka 23 hadi 50 ambao wangependa kuhudhuria shule hiyo wanaweza kupata habari zaidi katika mikutano inayofanywa na mwangalizi wa wilaya wakati wa kusanyiko la mzunguko. Lazima wawe wazee au wawe wametumikia wakiwa watumishi wa huduma kwa angalau miaka miwili mfululizo.
◼ Darasa la kwanza la Shule ya Waangalizi Wanaosafiri lilifanywa Februari 20 hadi Aprili 17, 2004. Madarasa mengine mawili yatafuata. Waangalizi wanaosafiri kutoka Burundi, Ethiopia, Kenya, Rwanda, Sudan, Tanzania, na Uganda watahudhuria.
◼ Kuanzia Juni, fomu za kila mwaka zitatiwa ndani ya upakizi wa vichapo wa kutaniko zikipatikana. Maagizo kuhusu jinsi ya kuzigawanya fomu hizo yatapatikana kwenye orodha ya upakizi. Ikiwa makutaniko kadhaa yanatumia Jumba moja la Ufalme, mratibu wa vichapo anapaswa kuhakikisha kwamba kila kutaniko linapokea fomu zake mara tu zifikapo.