Pitio La Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi
Maswali yafuatayo yatashughulikiwa kwa njia ya maswali na majibu katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanzia Juni 28, 2004. Mwangalizi wa shule ataongoza pitio la dakika 30 linalotegemea habari zilizozungumziwa kwenye hotuba zilizotolewa kuanzia juma la Machi 1 hadi Juni 28, 2004. [Taarifa: Mahali ambapo vitabu vya marejeo havijatajwa baada ya swali, utahitaji kufanya utafiti wako mwenyewe ili kupata majibu.—Ona Shule ya Huduma, uku. 36-37.]
SIFA ZA USEMI
1. Ni mambo gani yanayoweza kutufanya tutoe hotuba kwa njia isiyo ya maongezi au iliyo rasmi kupita kiasi? [be uku. 179 fu. 4]
2. Kwa nini kuboresha sauti yetu hakutegemei tu kupumua vizuri na kutuliza misuli? [be uku. 181 fu. 2]
3. Tunapowafundisha watu kweli za Biblia, ni mambo gani tunayoweza kufanya ili ‘tuwe mambo yote kwa watu wa namna zote’? (1 Kor. 9:20-23) [be uku. 186 fu. 2-4]
4. Kusikiliza kwa makini katika huduma yetu kunatia ndani mambo gani? [be uku. 187]
5. Kwa nini ni muhimu kumheshimu kila mtu tunayekutana naye katika huduma yetu? [be uku. 190]
HOTUBA NA. 1
6. Wale wanaofundisha maagizo ya Mungu wana mradi gani, na ni nini kitakachotusaidia kuufikia mradi huo? (Mt. 5:16; Yoh. 7:16-18) [be uku. 56 fu. 3–uku. 57 fu. 2]
7. Kwa nini ni muhimu kuonyesha tofauti zilizoko kati ya mambo unapofundisha, na Yesu alitumiaje mbinu hii ya kufundisha? [be uku. 57 fu. 3; uku. 58 fu. 2]
8. Tofauti na Mafarisayo, mafundisho ya Yesu yaliifikiaje mioyo ya watu? [be uku. 59 fu. 2-3]
9. Tunawezaje kuwasaidia wanafunzi watumie mambo wanayojifunza, bila kuwafanyia maamuzi? [be uku. 60 fu. 1-3]
10. Tunapaswa kuwajibuje watu wanaouliza maswali kuhusu maamuzi ya kibinafsi? [be uku. 69 fu. 4-5]
USOMAJI WA BIBLIA WA KILA JUMA
11. Kwa nini Musa alipaswa kufuata kwa uangalifu “mfano wa maskani na mfano wa vyombo vyake vyote”? (Kut. 25:9) [it-2 uku. 1058 fu. 7]
12. Tunajifunza nini kutokana na jibu la Haruni kwa Musa katika kisa cha ndama wa dhahabu? (Kut. 32:24)
13. Tunajifunza nini kutokana na imani waliyoonyesha Waisraeli walipotii amri ya Yehova katika Kutoka 34:23, 24?
14. Dhabihu ya ushirika ilitolewa kwa kusudi gani? (Law. 3:1)
15. Utaratibu wa kumweka rasmi Haruni, unaotajwa katika Mambo ya Walawi 8:23, ulimhusuje Yesu? [it-2 uku. 1113 fu. 4; w68 uku. 399 fu. 24 (Kiingereza)]