Matangazo
◼ Toleo la vichapo la Julai na Agosti: Broshua yoyote kati ya broshua zifuatazo zenye kurasa 32 yaweza kutumiwa: Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je! Uamini Utatu?, Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote? Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Ni Nini Hutupata Tunapokufa?, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?, Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli?, Serikali Itakayoleta Paradiso, “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya,” na Our Problems—Who Will Help Us Solve Them? Septemba: Kitabu Je, Kuna Muumba Anayekujali? Pia unaweza kutoa kitabu Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation? (kikubwa au kidogo) badala yake, au Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu! Oktoba: Kampeni ya pekee ya kugawanya broshua mpya, lakini nakala mojamoja za Mnara wa Mlinzi na Amkeni! zitatolewa mwezi wote. Habari zaidi zitatolewa baadaye ili kuhakikisha kwamba ugavi wa kawaida wa magazeti umetumiwa wote. Mahali ambapo kuna mtu anayependezwa, tafadhali toa broshua Anataka, na ufuatie ukiwa na mradi wa kuanzisha mafunzo ya Biblia.
◼ Kuanzia Septemba, waangalizi wa mzunguko watatoa hotuba ya watu wote yenye kichwa “Kukabili Wakati Ujao kwa Imani na Ujasiri.”
◼ Wahubiri wanaweza kutoa broshua Anataka au kitabu Ujuzi wanapohubiri maeneo yasiyogawiwa mtu. Kitabu kingine chochote kinaweza kutolewa ikiwa mwenye nyumba tayari ana vichapo hivyo viwili. Wote wanapaswa kubeba trakti mbalimbali kwa ajili ya watu wasiopatikana nyumbani au watu wasiokubali vichapo vyetu. Tunapaswa kujitahidi kufuatia upendezi, hasa mahali ambapo maeneo yasiyogawiwa mtu yako karibu na makutaniko.
◼ Waandishi wa makutaniko wanapaswa kuwa na fomu za kutosha za Ombi la Utumishi wa Painia wa Kawaida (S-205) na Ombi la Utumishi wa Painia-Msaidizi (S-205b). Fomu hizi zinaweza kuagizwa kupitia Fomu ya Kuomba Vitabu (S-14). Wekeni angalau za mwaka mzima.
◼ Kabla ya mwandishi kutuma fomu za maombi ya painia wa kawaida kwenye ofisi ya tawi, anapaswa kuzipitia fomu hizo na kuhakikisha kwamba zimejazwa kikamili. Ikiwa wenye kujaza ombi hilo hawakumbuki tarehe yao ya ubatizo, wanaweza kuikadiria na kuiandika mahali. Mwandishi anapaswa kuandika tarehe hiyo kwenye kadi ya Rekodi ya Kutaniko ya Mhubiri.
◼ Iwapo wakati wowote utapanga kusafiri nchi nyingine, na utake kufahamishwa tarehe, wakati, na mahali pa kuhudhuria mikutano ya kutaniko, kusanyiko la mzunguko au la wilaya, uliza ofisi ya tawi inayosimamia kazi katika nchi hiyo. Utapata orodha ya anwani za ofisi ya tawi katika ukurasa wa mwisho wa Kitabu cha Mwaka cha karibuni.
◼ Ni lazima ofisi ya tawi iwe na anwani na namba za simu za karibuni za waangalizi-wasimamizi na waandishi wote. Ikiwa kutakuwa na badiliko lolote, Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko yapaswa kujaza, kutia sahihi na kutuma fomu ya Badiliko la Anwani ya Mwangalizi-Msimamizi/Badiliko la Anwani ya Mwandishi (S-29) kwa ofisi ya tawi haraka iwezekanavyo. Fomu hiyo yapasa kutumwa ikiwa kuna mabadiliko yoyote ya namba ya simu ya eneo lao.