Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/04 uku. 7
  • Matangazo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Matangazo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 12/04 uku. 7

Matangazo

◼ Toleo la vichapo la Desemba: Toa kitabu, Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi au vichapo vingine kama vile, Biblia—Neno la Mungu au la Mwanadamu, Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia, na Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. Januari: Kitabu chochote chenye kurasa 192 kilichochapishwa kwenye karatasi inayochujuka au kugeuka rangi na kuwa manjano au kitabu chochote kilichochapishwa kabla ya 1990 chaweza kutolewa, na pia Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Makutaniko ambayo hayana vitabu hivyo vya zamani yanaweza kutoa kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu. Februari: Kitabu Mkaribie Yehova. Machi: Toa broshua Endeleeni Kukesha. Ikiwa mtu anapendezwa kikweli, mwonyeshe kitabu Ujuzi ukiwa na kusudi la kuanzisha funzo la Biblia.

◼ Makala za mwanzo kuhusu, “Kumwelewa Daktari” katika toleo la Amkeni! la Januari 22, 2005, zinakusudiwa kuwasaidia watu wawe na uelewevu zaidi wanaposhughulika na madaktari. Hata hivyo, makala hizo zitawapendeza madaktari, kwa kuwa zinazungumzia sababu ambazo zimefanya madaktari kadhaa wavutiwe na ujumbe wa tumaini wa Biblia. Huenda ukataka kuagiza nakala zaidi za gazeti hilo na kujitahidi kuwapa madaktari na pia wataalamu wengine wa afya. Makutaniko yanapaswa kuwasiliana na ofisi ya tawi bila kukawia ikiwa yanahitaji nakala zaidi za gazeti hilo.

◼ Mialiko ya Ukumbusho ya 2005 katika lugha kuu ya kila kutaniko itatumwa hivi karibuni. Ikiwa kuna lugha nyingine katika eneo lenu na mngependa mialiko katika lugha hizo, agizeni mialiko hiyo haraka iwezekanavyo mkitumia Fomu ya Kuomba Vitabu (S-14). Katika eneo letu mialiko hiyo ya Ukumbusho itapatikana katika Kiarabu, Kiganda, Kiingereza, Kirundi, Kiswahili. Tafadhali ombeni tu lugha zile zinazohitajiwa katika eneo lenu.

◼ Tungependa kuwajulisha kwamba Ukumbusho wa mwaka wa 2006 utakuwa Jumatano, Aprili 12, baada ya jua kutua. Taarifa hii imetolewa mapema ili akina ndugu waweze kufanya mapatano ya kukodi majumba mengine mahali ambapo makutaniko kadhaa yanatumia Jumba moja la Ufalme. Wazee wanapaswa kufanya maagano pamoja na wasimamizi wa jumba watakalokodi ili kuhakikisha kwamba Ukumbusho unaadhimishwa kwa njia ya amani na kwa utaratibu bila kuvurugwa na utendaji mwingine katika jengo hilo.

◼ Kwa sababu Ukumbusho ni tukio muhimu, baraza la wazee linapaswa kumteua mzee anayestahili zaidi atoe hotuba ya Ukumbusho badala ya kupokezana zamu tu au kutumia ndugu yuleyule kila mwaka. Ikiwa kuna mzee mwenye uwezo ambaye ni mtiwa-mafuta, apewe mgawo huo.

◼ Kuanzia juma la Juni 27, 2005, tutajifunza kitabu Sikiliza Unabii wa Danieli! kwenye Funzo la Kitabu la Kutaniko.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki