Pitio La Shule Ya Huduma Ya Kitheokrasi
Maswali yafuatayo yatashughulikiwa kwa njia ya maswali na majibu katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanza Aprili 25, 2005. Mwangalizi wa shule ataongoza pitio la dakika 30 linalotegemea habari zilizozungumziwa katika hotuba ambazo zilitolewa kuanzia juma la Machi 7 hadi Aprili 25, 2005. [Taarifa: Mahali ambapo vichapo vya marejeo havijaonyeshwa baada ya swali, utahitaji kufanya utafiti wako mwenyewe ili kupata majibu.—Ona Shule ya Huduma, uku. 36-37.]
SIFA ZA USEMI
1. Tunapotayarisha hotuba, tunawezaje kutumia vizuri habari tuliyopewa, na kwa nini jambo hilo ni muhimu? [be uku. 234 fu. 1-3, masanduku]
2. Tunapotoa hotuba, tunapaswa kutumia kiasi gani cha habari tuliyopewa? [be uku. 234 fu. 4–uku. 235 fu. 1]
3. Tunawezaje kutumia maswali ili kuchochea mazungumzo tunapohubiri? (Mdo. 8:30) [be uku. 236 fu. 2-5]
4. Tunawezaje kutumia maswali ili kuwasaidia wanafunzi wa Biblia watumie ‘nguvu zao za kufikiri’? (Rom. 12:1) [be uku. 238 fu. 1]
5. Maswali yaliyoulizwa kwenye Waroma 8:31, 32 na Isaya 14:27 yana matokeo gani? [be uku. 238 fu. 6–uku. 239 fu. 1]
HOTUBA NA. 1
6. ‘Tunamwekaje Kristo kuwa msingi’ katika kazi yetu ya kufanya wanafunzi? (1 Kor. 3:11) [be uku. 278 fu. 1-2]
7. Kwa kuwa Yehova alimpa Mwana wake mamlaka kamili ya utawala mwaka wa 1914, kusudi letu ni nini tunaposali, “Ufalme wako na uje”? (Mt. 6:9, 10) [be uku. 279 fu. 4]
8. Kwa nini Wakristo wote wanapaswa kujifunza kusoma, na Yesu aliweka kielelezo gani kuhusu jambo hilo? [w03 3/15 uku. 10 fu. 5; uku. 12 fu. 2]
9. Kielelezo cha Yosia na Yesu kinawezaje kuwasaidia vijana wafanye maendeleo ya kiroho? [w03 4/1 uku. 8 fu. 3-4; uku. 10 fu. 3]
10. Kwa nini tunaweza kumtumaini Mungu? (Met. 3:5, 6, Union Version) [w03 11/1 uku. 4 fu. 6-7]
USOMAJI WA BIBLIA KILA JUMA
11. Kwa nini Hana alisali kwamba Yehova “ampe mfalme wake nguvu” ingawa wakati huo hakukuwa na mfalme wa kibinadamu aliyetawala Israeli? (1 Sam. 2:10)
12. Tunaweza kujifunza nini kutokana na ukweli wa kwamba Waisraeli walishindwa hata ingawa walikuwa na sanduku la agano? (1 Sam. 4:3, 4, 10)
13. Kwa nini andiko la 1 Mambo ya Nyakati 2:13-15 humtaja Daudi kuwa mwana wa saba wa Yese, ilhali 1 Samweli 16:10, 11 linaonyesha kwamba alikuwa wa nane?
14. Ni “roho mbaya” gani iliyomtia hofu Sauli? (1 Sam. 16:14)
15. Je, ule ubashiri uliotolewa na “Samweli” kupitia mwanamke mwenye kuwasiliana na pepo huko En-dori ulikuwa wa kweli? (1 Sam. 28:16-19)