Matangazo
◼ Aprili na Mei: Tutatoa magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Unapowarudia watu wanaopendezwa, watembelee pia wale ambao huhudhuria ukumbusho na/au mkutano mwingine lakini ambao hawashirikiani na kutaniko kwa ukawaida na ujitahidi kuwatolea kitabu Mwabudu Mungu. Lengo lako lapaswa kuwa kuanzisha funzo la Biblia, hasa na wale ambao tayari wamejifunza kitabu Ujuzi na broshua Anataka. Juni: Toa kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu, lakini mwenye nyumba akisema hana watoto mtolee kitabu Ujuzi. Jitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia. Julai: Broshua yoyote kati ya zile zifuatazo zenye kurasa 32 yaweza kutolewa: Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je! Uamini Utatu?, Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Ni Nini Hutupata Tunapokufa?, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?, Serikali Itakayoleta Paradiso, na “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya.” Huenda broshua zifuatazo zikafaa katika sehemu fulani za eneo lenu: Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?, Jinsi ya Kupata Maisha Yenye Kuridhisha, Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli?, na Our Problems—Who Will Help Us Solve Them?
◼ Kuanzia Juni, beji za kusanyiko la wilaya la 2005 zitatumwa kwa makutaniko. Makutaniko yaliyo na kikundi cha lugha ya kigeni ndiyo tu yanayohitaji kuagiza beji hizo. Beji hupakiwa katika mafungu yenye kadi 25, na idadi ya beji zitatumwa ikitegemea idadi ya wahubiri kutanikoni. Ikiwa kutaniko linahitaji beji zaidi, zinaweza kuagizwa kwenye Fomu ya Kuomba Vitabu (S-14). Mnapaswa kuagiza vifuko vya plastiki vya beji kwa ajili ya yeyote kutanikoni anayevihitaji.
◼ Ofisi ya tawi inapaswa kuwa na anwani na namba za simu za karibuni za waangalizi-wasimamizi na waandishi wote. Julisheni ofisi ya tawi haraka iwezekanavyo kuhusu mabadiliko yoyote ya anwani au namba za simu. Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko inapaswa kujaza Fomu ya Badiliko la Anwani ya Mwangalizi-Msimamizi/Badiliko la Anwani ya Mwandishi (S-29). Pia fomu hiyo inapaswa kutumwa ikiwa kuna mabadiliko yoyote katika namba ya simu ya eneo.
◼ Waandishi wa makutaniko wanapaswa kuwa na fomu za kutosha za Ombi la Utumishi wa Painia wa Kawaida (S-205) na Ombi la Utumishi wa Painia-Msaidizi (S-205b). Mnaweza kuagiza fomu hizo kwenye Fomu ya Kuomba Vitabu (S-14). Wekeni akiba ya angalau mwaka mmoja. Pitieni fomu zote za ombi la painia wa kawaida ili kuhakikisha kwamba zimejazwa kikamili.