Matangazo
◼ Agosti: Broshua yoyote kati ya broshua zifuatazo zenye kurasa 32 yaweza kutumiwa: Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je! Uamini Utatu?, Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Ni Nini Hutupata Tunapokufa?, Mungu Anataka Tufanye Nini?, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?, Serikali Itakayoleta Paradiso, na “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya.” Broshua zifuatazo zinaweza kufaa katika maeneo fulani: Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?, Jinsi ya Kupata Maisha Yenye Kuridhisha, Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli?, na Our Problems—Who Will Help Us Solve Them? Kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele kinaweza pia kutolewa, hasa katika maeneo ya mbali. Septemba: Kitabu Je, Kuna Muumba Anayekujali?, Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele, broshua yenye kurasa 32 Endeleeni Kukesha!, au vitabu vingine vya zamani ambavyo viko kutanikoni vinaweza kutolewa. Oktoba: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! yatatolewa mwezi wote. Tafadhali wape watu wanaopendezwa broshua Anataka, na uwarudie ukiwa na lengo la kuanzisha mafunzo ya Biblia. Novemba: Toa kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu. Mwenye-nyumba akisema kwamba hana watoto, mtolee kitabu Ujuzi au trakti Je, Ungependa Kujua Mengi Zaidi Kuhusu Biblia?
◼ Kwa kuwa mwezi wa Oktoba una miisho-juma mitano, huo ni mwezi mzuri sana wa kufanya upainia msaidizi.
◼ Ukurasa wa 5 na wa 6 wa toleo hili la Huduma Yetu ya Ufalme unapaswa kuwekwa na kutumiwa kuhusiana na programu ya kusanyiko la mzunguko na la pekee la mwaka wa utumishi wa 2006.
◼ Mwangalizi msimamizi au mtu fulani aliyeteuliwa naye anapaswa kukagua hesabu ya kutaniko Septemba 1 au upesi iwezekanavyo baada ya tarehe hiyo. Ikiwa kuna akaunti ya benki ya kushughulikia udumishaji au ujenzi wa Jumba la Ufalme, fanyeni mipango ili akaunti hiyo ikaguliwe pia. Ukaguzi huo unapokamilishwa, kutaniko linapaswa kutangaziwa jambo hilo wakati ripoti ya hesabu inaposomwa.
◼ Tunawakumbusha kwamba hampaswi kamwe kutumia anwani ya ofisi ya tawi kwenye barua za kibinafsi. Hilo linatia ndani barua zote na vichapo ambavyo vinatumwa kwa watu wanaopendezwa, kwa wale wasio nyumbani, au wale wanaoishi katika sehemu ambazo hazifikiki kwa urahisi. Mhubiri anaweza kuandika anwani yake ili itumiwe kujibu barua, kwa kuwa huduma yake ni sehemu ya utumishi wake kwa Mungu. (Mt. 28:19, 20; Rom. 10:14, 15) Hata hivyo, ikiwa anahisi kwamba si jambo la hekima kutumia anwani yake anapohubiri kupitia barua, anaweza kutumia jina lake na anwani ya Jumba la Ufalme.—Ona Sanduku la Swali katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Desemba 2002.
◼ Makutaniko yanapaswa kuanza kuagiza Kalenda ya Mwaka wa 2006 ya Mashahidi wa Yehova, Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2006, na Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova cha 2006 katika ombi lao la vichapo litakalofuata. Makutaniko yatapokea orodha ya lugha ambazo vichapo hivyo vinapatikana.