Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/06 uku. 4
  • Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Huduma ya Ufalme—2006
Huduma ya Ufalme—2006
km 4/06 uku. 4

Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi

Maswali yafuatayo yatashughulikiwa kwa njia ya maswali na majibu katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanza Aprili 24, 2006. Mwangalizi wa shule ataongoza pitio la dakika 30 linalotegemea habari zilizozungumziwa katika hotuba ambazo zilitolewa kuanzia juma la Machi 6 hadi Aprili 24, 2006. [Taarifa: Mahali ambapo vichapo vya marejeo havijaonyeshwa baada ya swali, utahitaji kufanya utafiti wako mwenyewe ili kupata majibu.—Ona Shule ya Huduma, uku. 36-37.]

SIFA ZA USEMI

1. Tunapofundisha, kwa nini tunapaswa kutua tunapobadili mawazo, lakini ni nini kinachoweza kutuzuia tusitue? [be uku. 98 fu. 2-3]

2. Kwa nini ni muhimu kutua tunapowahubiria watu? [be uku. 99 fu. 5–uku. 100 fu. 4]

3. Kwa nini ni muhimu kukazia maana tunapotoa hotuba, na tunawezaje kukazia maana ifaavyo? [be uku. 101 fu. 1-5, sanduku]

4. Tunaposoma mbele ya watu, tunawezaje kuhakikisha kwamba tunakazia mambo makuu ya habari tunayosoma? [be uku. 105 fu. 1-6]

5. Kwa nini ni muhimu kutumia kiasi kinachofaa cha sauti tunapofundisha, na tunawezaje kujua kama tunafanya hivyo? [be uku. 107-108]

HOTUBA NA. 1

6. Hali ya Wakristo leo inafananaje na ile ya Esta na Mordekai, na tunawezaje kuwaiga? [si uku. 94 fu. 17]

7. Sulemani alikuwa akifafanua nini aliposema kwamba “kila kitu kilikuwa ubatili na kufuatilia upepo”? (Mhu. 2:11) [w04 10/15 uku. 4 fu. 3-4]

8. Tunawezaje kusitawisha upendo kwa Mungu? (Marko 12:30) [w04 3/1 uku. 19-21]

9. Kuna tofauti gani kati ya kupenda kanuni za kiroho na kupenda mali? [w04 10/15 uku. 5-7]

10. Ni mambo gani yanayoweza kutusaidia kusikiliza bila kukengeushwa tunapokuwa makusanyikoni? [be uku. 15-16]

USOMAJI WA BIBLIA WA KILA JUMA

11. Kwa nini uso wa Hamani ulifunikwa? (Esta 7:8)

12. Ni kiumbe wa roho wa aina gani aliyeathiri kufikiri kwa Elifazi? (Ayu. 4:15, 16) [w05 9/15 uku. 26 fu. 2]

13. Je, maneno ya Ayubu 7:9, 10 na 10:21 yanaonyesha kwamba Ayubu hakuamini ufufuo?

14. Huenda Ayubu alimaanisha nini aliposema “ninaponyoka na ngozi ya meno yangu”? (Ayu. 19:20)

15. Ayubu alimaanisha nini aliposema, “sitajiondolea utimilifu wangu,” na maneno hayo yanatufundisha nini? (Ayu. 27:5)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki