Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/06 uku. 3
  • Matangazo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Matangazo
  • Huduma ya Ufalme—2006
Huduma ya Ufalme—2006
km 5/06 uku. 3

Matangazo

Mei: Tutatoa magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Tunapowarudia watu wenye kupendezwa, kutia ndani wale ambao huhudhuria ukumbusho na/au mikutano mingine ya pekee lakini hawashirikiani sana na kutaniko, tutawatolea hasa kile kitabu kipya Biblia Inafundisha Nini Hasa? Lengo lako lapaswa kuwa kuanzisha funzo la Biblia kwa kutumia kitabu hicho. Juni: Toa kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu, lakini mwenye nyumba akisema hana watoto mtolee kitabu Ujuzi. Jitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia. Julai na Agosti: Broshua yoyote kati ya zile zifuatazo zenye kurasa 32 yaweza kutolewa: Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je! Uamini Utatu?, Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Mungu Anataka Tufanye Nini?, Ni Nini Hutupata Tunapokufa?, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?, Serikali Itakayoleta Paradiso, na “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya.” Huenda broshua zifuatazo zikafaa katika sehemu fulani za eneo lenu: Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?, Jinsi ya Kupata Maisha Yenye Kuridhisha, Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli?, na Our Problems—Who Will Help Us Solve Them?

◼ Kwa kuwa mwezi wa Julai una miisho-juma mitano, huo ni mwezi mzuri sana wa kufanya upainia msaidizi.

◼ Mwangalizi-msimamizi au ndugu fulani aliyeteuliwa naye anapaswa kukagua hesabu za kutaniko mnamo Juni 1, au upesi iwezekanavyo baada ya tarehe hiyo. Ikiwa kuna akaunti nyingine ya benki, kama vile akaunti ya ujenzi au ya udumishaji wa Jumba la Ufalme, mipango inapaswa kufanywa ili kuzikagua. Ukaguzi ukikamilishwa, kutaniko linapaswa kutangaziwa ripoti ya ukaguzi pamoja na ripoti ya hesabu itakayofuata.

◼ TAARIFA YA PEKEE: Hundi zinazotolewa kama michango katika kusanyiko la wilaya na zile zinazopelekwa kwenye ofisi ya tawi ziandikishwe kwa jina la shirika linalotambuliwa kisheria katika nchi yenu.

◼ Inapendekezwa kwamba fomu ya ombi la upainia wa kawaida itumwe kwenye ofisi ya tawi angalau siku 30 kabla ya tarehe ambayo mtu anatazamia kuanza upainia. Mwandishi wa kutaniko anapaswa kuchunguza fomu ya ombi ili kuhakikisha kwamba imejazwa kikamili. Ikiwa wahubiri wanaotoa ombi hawakumbuki tarehe hususa waliyobatizwa, wanapaswa kukadiria tarehe hiyo na kuiandika ili waitumie kwa ukawaida kama tarehe yao ya ubatizo. Mwandishi anapaswa kuandika tarehe hiyo katika kadi ya Rekodi ya Kutaniko ya Mhubiri (S-21).

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki