Matangazo
◼ Juni: Toa kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu, lakini mwenye nyumba akisema hana watoto, mtolee kitabu Ujuzi. Jitahidi kuanzisha mafunzo ya Biblia. Julai na Agosti: Broshua yoyote kati ya zile zifuatazo zenye kurasa 32 inaweza kutolewa: Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je! Uamini Utatu?, Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Mungu Anataka Tufanye Nini?, Ni Nini Hutupata Tunapokufa?, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?, Serikali Itakayoleta Paradiso, na “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya.” Septemba: Tutatoa kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? Tunapaswa kujitahidi sana kuanzisha mafunzo ya Biblia katika ziara ya kwanza. Unapaswa kufanya ziara za kurudia kila mahali ambapo kitabu kiliachwa ukiwa na lengo la kuanzisha funzo la Biblia.
◼ Kwa kuwa mwezi wa Julai una miisho-juma mitano, huo ni mwezi mzuri sana wa kufanya upainia msaidizi.
◼ Video Young People Ask—How Can I Make Real Friends? Itazungumziwa katika Mkutano wa Utumishi mwezi wa Septemba. Ikiwa mnahitaji video hiyo, mnaweza kuomba nakala kupitia kutaniko haraka iwezekanavyo. Mahali ambapo hakuna video hiyo, habari iliyo kwenye sura ya 8, ukurasa wa 65, ya kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, itazungumziwa. Wote wanaweza kuombwa wasome sura hiyo.