Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 7/06 uku. 3
  • Matangazo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Matangazo
  • Huduma ya Ufalme—2006
Huduma ya Ufalme—2006
km 7/06 uku. 3

Matangazo

◼ Julai na Agosti: Broshua yoyote kati ya zile zifuatazo zenye kurasa 32 inaweza kutolewa: Furahia Milele Maisha Duniani!, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je! Uamini Utatu?, Endeleeni Kukesha!, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Mungu Anataka Tufanye Nini?, Ni Nini Hutupata Tunapokufa?, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje?, Serikali Itakayoleta Paradiso, na “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya.” Katika sehemu fulani ya eneo letu huenda ikafaa kutoa broshua zifuatazo: Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?, Jinsi ya Kupata Maisha Yenye Kuridhisha, Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, Our Problems—Who Will Help Us Solve Them? na Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli? Kitabu Ujuzi kinaweza kutolewa pia. Septemba: Tutatoa kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? Tunapaswa kujitahidi sana kuanzisha mafunzo ya Biblia katika ziara ya kwanza. Unapaswa kufanya ziara za kurudia kila mahali ambapo kitabu kiliachwa ukiwa na lengo la kuanzisha funzo la Biblia. Oktoba: Tutatoa magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! yakiwa pamoja. Mtu akipendezwa, tafadhali mwonyeshe broshua Endeleeni Kukesha! ili kumchochea apendezwe zaidi na Biblia.

◼ Kuanzia Septemba, waangalizi wa mzunguko watatoa hotuba yenye kichwa “Una Msimamo Gani Mbele za Mungu?”

◼ Kuanzia juma la Januari 8, 2007, tutajifunza Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu! katika Funzo la Kitabu la Kutaniko. Chapa kubwa ya kitabu hicho inatayarishwa sasa. Makutaniko yanapaswa kuwa na nakala za kutosha za chapa ya kawaida na chapa kubwa kabla ya wakati huo.

◼ Inapendekezwa kwamba fomu ya ombi la upainia wa kawaida itumwe kwenye ofisi ya tawi angalau siku 30 kabla ya tarehe ambayo mtu anatazamia kuanza upainia. Mwandishi wa kutaniko anapaswa kuchunguza fomu ya ombi ili kuhakikisha kwamba imejazwa kikamili. Ikiwa wahubiri wanaotoa ombi hawakumbuki tarehe hususa waliyobatizwa, wanapaswa kukadiria tarehe hiyo na kuiandika ili waitumie kwa ukawaida kama tarehe yao ya ubatizo. Mwandishi anapaswa kuandika tarehe hiyo iliyokadiriwa katika kadi ya Rekodi ya Kutaniko ya Mhubiri (S-21).

◼ Waandishi wa makutaniko wanapaswa kuhakikisha kwamba wana Barua ya Kuwekwa Rasmi kwa Painia (S-202) kwa ajili ya kila painia wa kawaida kutanikoni. Ikiwa hawana barua hiyo, tafadhali andikieni ofisi ya tawi kuhusu jambo hilo. Painia wa kawaida anapohama kutaniko, mwandishi anapaswa kufuata kwa uangalifu maagizo yaliyo nyuma ya barua ya S-202.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki