Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/06 uku. 3
  • Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Huduma ya Ufalme—2006
Huduma ya Ufalme—2006
km 8/06 uku. 3

Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi

Maswali yafuatayo yatashughulikiwa kwa njia ya maswali na majibu katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanza Agosti 28, 2006. Mwangalizi wa shule ataongoza pitio la dakika 30 linalotegemea habari zilizozungumziwa katika hotuba ambazo zilitolewa kuanzia juma la Julai 3 hadi Agosti 28, 2006. [Taarifa: Mahali ambapo vichapo vya marejeo havijaonyeshwa baada ya swali, utahitaji kufanya utafiti wako mwenyewe ili kupata majibu.—Ona Shule ya Huduma, uku. 36-37.]

SIFA ZA USEMI

1. Kuwatazama wasikilizaji hutusaidiaje kuwa walimu bora? (Mt. 19:25, 26; Mdo. 14:9, 10) [be uku. 124 fu. 3–uku. 125 fu. 3]

2. Kwa nini ni muhimu kuzungumza kwa njia ya kawaida, na ni mambo gani yanaweza kutusaidia kufanya hivyo tunapokuwa katika huduma ya shambani? [be uku. 128 fu. 1–5, sanduku]

3. Kwa nini tunapaswa kuwa nadhifu na safi? [be uku. 131 fu. 1-3]

4. Kuwa na “kiasi na utimamu wa akili” kunapaswa kuathirije jinsi tunavyovaa na kujipamba? (1 Tim. 2:9) [be uku. 131 fu. 4–uku. 132 fu. 1]

5. Tunapaswa kufuata kanuni gani za Biblia ili kuhakikisha kwamba jinsi tunavyovalia hakuonyeshi kwamba tunaupenda ulimwengu? [be uku. 133 fu. 2-3]

HOTUBA NA. 1

6. Kusoma kunatokeza manufaa gani kubwa? [be uku. 21 fu. 3]

7. Ni nini huamua kama mtu ni mwenye hekima au ni mpumbavu? (Met. 14:2) [w04 11/15 uku. 26 fu. 5]

8. Kwa nini ‘ujuzi ni jambo rahisi kwa mtu mwenye uelewaji’? (Met. 14:6) [w04 11/15 uku. 28 fu. 4-5]

9. Funzo ni nini? [be uku. 27 fu. 3]

10. Kutafakari kazi za uumbaji za Yehova kunapaswa kuwe na matokeo gani kwetu? [w04 11/15 uku. 8 fu. 4]

USOMAJI WA BIBLIA WA KILA JUMA

11. Katika nyakati za kale, Yehova ‘alisema’ neno gani ambalo lilifanya jeshi kubwa la ‘wanawake litangaze habari njema,’ na hilo linatimizwaje leo? (Zab. 68:11)

12. Ni nini karibu kimfanye Asafu aache kutenda mema, na fikira zake zilirekebishwaje? (Zab. 73:2, 3, 17)

13. Kwa nini mana ambayo Waisraeli walipewa iliitwa “nafaka ya mbinguni” na “mkate wa wenye nguvu”? (Zab. 78:24, 25)

14. Ni nini “mahali pa siri pa Aliye Juu Zaidi,” nasi tunaweza ‘kukaaje’ humo? (Zab. 91:1, 2)

15. Ni katika njia gani kifo cha washikamanifu wa Yehova ni chenye thamani machoni pake? (Zab. 116:15)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki