Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 10/06 uku. 7
  • Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Huduma ya Ufalme—2006
Huduma ya Ufalme—2006
km 10/06 uku. 7

Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi

Maswali yafuatayo yatashughulikiwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanza Oktoba 30, 2006. Mwangalizi wa shule ataongoza pitio la dakika 30 linalotegemea habari zilizozungumziwa katika hotuba ambazo zilitolewa kuanzia juma la Septemba 4 hadi Oktoba 30, 2006. [Taarifa: Mahali ambapo vichapo vya marejeo havijaonyeshwa baada ya swali, utahitaji kufanya utafiti wako mwenyewe ili kupata majibu.—Ona Shule ya Huduma, uku. 36-37.]

SIFA ZA USEMI

1. Kwa nini ni muhimu kuwa na utulivu unapozungumza, na tunaweza kupunguzaje wasiwasi wetu? [be uku. 135 fu. 5–uku. 137 fu. 2, masanduku]

2. Tunapoulizwa maswali kuhusu imani yetu, kwa nini nyakati zote tunapaswa kutumia Biblia kujibu? [be uku. 143 fu. 1-3]

3. Tunaweza kuboreshaje ustadi wetu wa kutumia Biblia? [be uku. 144, sanduku]

4. Kwa nini ni muhimu kutumia Biblia mara nyingi tunapofundisha katika huduma, na tunawezaje kuwasaidia wengine waitumie katika mikutano ya kutaniko? [be uku. 145-146, masanduku]

5. Sisi hutaka kutimiza mambo gani mawili tunapotoa utangulizi wa andiko? [be uku. 147 fu. 2]

HOTUBA NA. 1

6. Ni ujumbe gani wa maana unaopatikana katika Zaburi? [si uku. 104 fu. 23]

7. Kitabu cha Methali kiliandikwa na kukusanywa lini? [si uku. 107 fu. 5]

8. Methali ni nini, na kwa nini jina la Kiebrania la kitabu hicho linafaa? [si uku. 107 fu. 6]

9. Katika Methali 2:1-5, ni wazo gani linalotolewa na himizo la kuendelea kutafuta ujuzi, uelewaji, na utambuzi ‘kama fedha, na kama hazina zilizofichika’? [be uku. 38 fu. 4]

10. Kitabu cha Methali kinafunuaje kusudi lake lenye mafaa? [si uku. 109 fu. 19]

USOMAJI WA BIBLIA WA KILA JUMA

11. Daudi ‘alituliza na kuinyamazishaje nafsi yake kama mtoto aliyeachishwa kunyonya juu ya mama yake,’ nasi tunaweza kumwigaje? (Zab. 131:1-3)

12. Ni faraja gani tunayoweza kupata kutokana na maneno yaliyopuliziwa ya Zaburi 139:7-12?

13. Ni mifano gani ya ukuu wa Yehova inayotajwa katika Zaburi 145 ambayo tunaweza kutumia kumsifu katika sala na katika huduma? (Zab. 145:3)

14. Ni katika njia gani kumwogopa Yehova ni “mwanzo wa ujuzi” na “mwanzo wa hekima”? (Met. 1:7; 9:10)

15. Katika Methali 7:1, 2, ni nini kinachohusishwa na “maneno yangu” na “amri zangu”?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki