Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/06 uku. 5
  • Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Huduma ya Ufalme—2006
Huduma ya Ufalme—2006
km 12/06 uku. 5

Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi

Maswali yafuatayo yatashughulikiwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanza Desemba 25, 2006. Mwangalizi wa shule ataongoza pitio la dakika 30 linalotegemea habari zilizozungumziwa katika hotuba ambazo zilitolewa kuanzia juma la Novemba 6 hadi Desemba 25, 2006. [Taarifa: Mahali ambapo vichapo vya marejeo havijaonyeshwa baada ya swali, utahitaji kufanya utafiti wako mwenyewe ili kupata majibu.—Ona Shule ya Huduma, uku. 36-37.]

SIFA ZA USEMI

1. Ni mambo gani yatakayotusaidia kuchagua utangulizi unaofaa wa andiko? [be uku. 148 fu. 4–uku. 149 fu. 1]

2. Tunaweza kutumia njia gani kuhakikisha kwamba maneno yetu yanakaziwa kwa njia ifaavyo? [be uku. 151 fu. 4–uku. 152 fu. 3]

3. Kwa kuwa kufundisha wengine Neno la Mungu ni jambo zito sana, tunapaswa kufanya nini ili ‘kulitumia sawasawa neno la kweli’? (2 Tim. 2:15) [be uku. 153 fu. 1-3, sanduku; uku. 154 fu. 1-2]

4. Ni katika njia zipi tunaweza kuonyesha vizuri jinsi maandiko tunayosoma yanavyohusika? [be uku. 154 fu. 4–uku. 155 fu. 3]

5. Kwa nini ni muhimu kuonyesha wasikilizaji jinsi ya kutumia habari tunayotoa, na tunawezaje kufanya hivyo? [be uku. 157 fu. 1-4, sanduku; uku. 158 fu. 1]

HOTUBA NA. 1

6. Sulemani alikuwa mkutanishi katika maana gani? [si uku. 112 fu. 1-3]

7. Kitabu cha Mhubiri kinapatanaje na mafundisho ya Yesu? [si uku. 114 fu. 16]

8. Kuna uthibitisho gani juu ya Wimbo wa Sulemani kuwa sehemu ya maandiko? [si uku. 115 fu. 3-4]

9. Hati-kunjo ya Isaya ya Bahari ya Chumvi inatoaje uthibitisho wenye kusadikisha kwamba Biblia zetu leo zawakilisha maandishi ya awali yaliyopuliziwa na Mungu? [si uku. 118 fu. 6]

10. Ni nini kinaweza kumsaidia msemaji asiwe na maandishi mengi sana? [be uku. 42 fu. 1]

USOMAJI WA BIBLIA WA KILA JUMA

11. Ni katika njia gani “wale wanaomtafuta Yehova wanaweza kuelewa kila jambo”? (Met. 28:5)

12. ‘Kazi ngumu ya wajinga huwachoshaje’? (Mhu. 10:15)

13. Mwanamwali Mshulami alithibitikaje kuwa “bustani iliyowekewa boma,” naye anawawekea wanawake Wakristo ambao bado hawajaolewa kielelezo gani bora? (Wim. 4:12)

14. Kwa kuwaalika Waisraeli ‘wanyooshe mambo,’ je, Yehova alikuwa akionyesha kwamba alikuwa tayari kujadiliana na kufikia mapatano fulani na watu wake? (Isa. 1:18a)

15. Andiko la Isaya 11:6-9 lilitimizwaje nyakati za kale, na kuna utimizo gani mkubwa?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki